Bukobawadau

TAARIFA KUHUSU MAJERAHA YA SHEIKH PONDA ISSA PONDA KUTOKA MOI

Sheikh Ponda Issa Ponda (54) alipokelewa hapa taasisi ya tiba ya mifupa na upasuaji wa mishipa ya fahamu MOI jana tarehe 11/8/2013 saa 7.30 jioni akitokea hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya kupokelewa alionekana akiwa na majeraha chini ya bega la mkono wa kulia lililokuwa limeshonwa mbele na nyuma madaktari wetu walifanya uchunguzi na kushauri afanyiwe kipimo cha X-ray ili kubaini kama kuna mvunjiko kwenye sehemu ya jeraha tathimini ya madaktari baada ya kupata majibu ya X-ray ilionyesha alikuwa na mvunjiko bila mifupa kupishana vivyo hivyo kidonda hakikuwa katika hali nzuri licha ya tiba ya mwanzo na iliamuliwa afanyiwe upasuaji mpya ili kuzuia maambukizi kama kingeachwa hivyo.

KWA HIYO 
1- kufuatana na tiba ya awali aliyopata ikiwa ni pamoja na kushonwa jeraha kabla ya kufikishwa MOI imekuwa vigumu kujua kama jeraha lilisababishwa na kitu gani 
2- kipimo cha X-ray kilionyesha kwamba alikuwa amepata mvunjiko wa mfupa mkubwa wa bega bila mifupa kupishana
3- hivyo basi Sheikh Ponda Issa Ponda anaendelea na matibabu baada ya upasuaji.

Imetolewa na:
Mkurugenzi Mtendaji
Taasisi ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu MOI
Next Post Previous Post
Bukobawadau