Bukobawadau

CHADEMA IKO IMARA-LWAKATARE

Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama Chadema Wilfred Lwakatare amesema chama chake kimezidi kuwa imara baada ya kuchukua hatua ya kuwafukuza wasaliti mara moja walipobainika.

Kiongozi huyo anayeongoza Idara nyeti ya Kurugenzi ya Ulinzi na usalama ndani ya chama amesema Idara yake ya usalama iko makini sasa hivi kuliko wakati mwingine wowote.

Amesema wako Imara kulinda mali za chama na viongozi wake na kupokea maagizo yoyote yatakayoamuliwa na ngazi ya juu.

Lwakatare amesema si jambo la ajabu kufukuza wasaliti wanaokwenda kinyume na taratibu za chama.

Source:Mwananchi.
Next Post Previous Post
Bukobawadau