Bukobawadau

WANANCHI NGARA WAITISHIA HALMASHAURI YAO KWA KUGAWA ARDHI BILA KUWASHIRIKISHA

 Pichani ni mahudhurio ya wananchi katika mkutano wa hadhara
Na Shaaban ndyamukama December 18,2013
NGARA: SERIKALI ya kijiji cha Kasulo wilayani Ngara mkoani Kagera  imemkataa mwekezaji aliyepewa ardhi ekari 50 na  halmashauri ya wilaya   yao   kwa madai kuwa  wananchi  hawakushirikishwa wakati anaoneshwa ardhi na kuimiliki

Mwenyekiti wa kijiji cha kasulo Bw.  Yusuph Katura amtoa kauli hiyo jana kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi wake pamoja na  watu walio na mashamba katika msitu wa Lumasi  uliofanyika katika kitongoji cha Benaco wilayani humo

Bw. Katura amesema kuwa  uongozi wa kijiji na kata haukushirikishwa wakati mwekezaji ambaye ni kanisa la   ELCT KKKT katika kutoa eneo hilo ambapo alitakiwa kupaendelezwana kamati ya maendeleo ya kijiji na kuridhiwa na mkutano mkuu


Alisema  wanaogawa eneo hilo kutoka Halmashauri wamefika wilayani hapo baada ya wakimbizi kuondoka waliokuwa katika ardhi hiyo  na wananchi ndio walishiriki kupanda miti  ambapo mpaka sasa ni miaka 3 tangu apatiwe eneo hilo

“Kwa  ridhaa ya wananchi walio nichagua mwekezaji aondoke mara moja vinginevyo mkurugenzi ataona maamuzi ya wananchi hapo baadaye”Alisema
 
Alidai kuwa uoungozi wa kata ya kasulo unashikilia msimamo wake kuwa  na kwamba   msitu wa  Lumasi na ardhi ya eneo  hilo ni mali ya kijiji cha kasulo na kukataa kuwa halmashauri ya wilaya  haina ardhi wala msitu katika eneo hilo

Mkutano ulioitishwa na mkuu wa wilaya ya Ngara Costantine Kanyasu lakini kutokana na majukumu ya kiutendaji  katibu tarafa ya Nyamiaga  Bw. Godian Bagombweki ndiye alimwakilisha ambapo diwani wa kata ya Kasulo   Bw. Phillibart Kiiza amedai kuwa msimamo wa kata ni kwamba ardhi ni mali ya serikali ya kijiji

Bw. Kiiza amesema kuwa uongozi wa kata pamoja na serikali ya kijiji  cha kasulo wanapinga tamko la halmashauri ya wilaya lililotolewa na afisa mistu wa wilaya Ngara Bw. Philipo Ileta kuwa  halmashauri itaendelea kuvuna miti kwa miaka mitatu ijayo na kwamba hawatakubali suara hilo

“Naungana na wanachi wa kijiji cha Kasulo kwamba wakati  mwekezaji huyo anapata eneo hilo watendaji wa idara ya ardhi na misitu walifanya kinyume cha sheria ya ardhi  namba 4 na  5 ya mwaka 1999”.Alisema diwani huyo
 
Kwa upande wake mwakilishi wa mkuu wa wilaya ambaye alikuwa katibu tarafa ya Nyamiaga Bw. Godian Bagambweki amesema kuwa uongozi wa halmashauri unapaswa kutafakari maoni ya wananchi na kufanya makubaliano ili kumaliza mgogoro kabla ya kutokea kwa athari za uvunjifu wa Amani.
Next Post Previous Post
Bukobawadau