Bukobawadau

BABY MADAHA NA KAMPUNI YAKE WALAMBA DILI LA HELA NYINGI NA KUBWA ZAIDI AFRIKA MASHARIKI

Ile record label maarufu ya muziki afrika mashariki - candy n candy imechapa fimbo nyingine baada ya kufanya deal ya mtonyo mrefuu na kampuni maarufu ya kusambaza filamu afrika mashariki na kati, (Jina kapuni ) kwa ajili ya kusambaza filamu ya “The gal bladder” ambayo imechezwa na mwigizaji baby madaha akishirikiana na waigizaji wengine toka kenya.

Kama alivyonukuliwa toka mtandao mmoja maarufu wa habari Afrika Mashariki, msemaji wa kampuni hiyo amesema imekua neema kwao kufanya kazi na kampuni kubwa kama candy n candy films ya nchini kenya, na hiyo itapanua wigo wa ukuaji wa tasnia ya filamu afrika mashariki hususani kenya na tanzania..deal hiyo yenye thamani ya shilingi za kitanzania milioni mia mbili ( mil.200 )inakua moja ya mikataba minono zaidi kufanywa east africa kutoka kwa kampuni kwenda kwa kampuni kwenye upande wa filamu.

Hiyo inachukukuliwa kuwa moja la pigo la kukata na shoka kwa kampuni pinzani grandpa records nayo ya nchini kenya ambayo kwa muda mrefu imekuwa ndani ya tasnia ya burudani kwa takribani zaidi ya miaka kumi bila kuleta mabadiliko yoyote katika tasnia nzima ya burudani,jambo ambalo candy n candy imeweza kufanya ndani ya miezi mitano tu,katika kutengeneza muziki wa kimataifa bila kusahau project yao ya sasa “highly budget movie the gal bladder”….ni mfano wa kuigwa kutoka kwa candy n candy records label kuzalisha kampuni tanzu ndani yake ya candy n candy films ambayo itakuwa ikidili na filamu.

Mbali na hayo kampuni hii ina plans za kuanzisha kipindi matata cha runinga ambacho kitakua kikirushwa Afrika Mashariki yote ,ambapo kama kawaida huwa hawachezi mbali host wake atakua first lady wa candy n candy mwanamuziki,mwigizaji,mwanamitindo na mtangazaji baby madaha”the queen of swaggz”,ikumbukwe hivi karibuni alilamba mamilioni ya shilingi kupitia mkataba wake na kampuni hiyo.

kaaazi kweli kweli…….yetu macho wabongo mpoooo?????
Next Post Previous Post
Bukobawadau