Bukobawadau

HUKO BUNDO BABA WA MIAKA 54 AOA MTOTO WA MIAKA MINANE

Bunda. Polisi Wilaya ya Bunda, wanamshikilia baba mwenye umri wa miaka 54 kwa tuhuma kuoa mwanafunzi wa kike wa umri wa miaka minane.
Msimamizi wa Dawati la Jinsia katika Kituo Kikuu cha Polisi Bunda, Rita Charles alisema baba huyo mkazi wa Kijiji cha Nyaburundu wilayani Bunda alikamatwa jana akiwa anaishi na binti huyo (jina limehifadhiwa) kama mke wa nyumbani baada ya kutoa kishika uchumba kiasi cha Sh55,000 kwa wazazi wake.
Ilielezwa kuwa mwanaume huyo kabla ya kumwoa mtoto huyo aliyekuwa anasoma darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Nyaburundu, alimchumbia kwa wazazi wake na kutakiwa atoe ng’ombe watano za mahari ndipo akatoa kishika uchumba hicho na mtoto huyo kuondolewa shule. “Tulifanikiwa kumkamata mwanamume huyo baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema,” alisema Rita.
Alisema siku ya Mwaka Mpya, alichukuliwa na dada yake na kumpeleka kwa mume wake huyo ili aanze maisha ya ndoa.
Hata hivyo, alisema alipofika, usiku huo walilala kitanda kimoja wote watatu (baba muoaji, muolewaji na dada wa muolewaji) na kwamba mwanamume huyo alianza kufanya mapenzi na dada yake na baadaye akamgeukia ‘mkewe’ kuanza kumnyonya maziwa.
“Tulilala wote watatu na alifanya mapenzi na dada yangu, mimi akininyonya maziwa,”
MWANANCHI
Next Post Previous Post
Bukobawadau