Bukobawadau

TISHIO LA KUONEKANA BOMU LALETA HALI YA TAHARUKI ENEO LA SHEKILANGO

Taharuki imewakumba baadhi ya wapita njia na wafanyabiashara katika makutano ya barabara ya Morogoro na Shekilango jijini Dar es salaam,na kusababisha baadhi ya shughuli kusimama baada ya wapita njia wawili kuona kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu la kutupwa kwa mkono huku baadhi ya askari polisi wakiwa na kazi ya ziada ya kuwaondoa baadhi ya wananchi waliokuwa wakitaka kushuhudia kitu hicho.

Tukio hilo limevutia hisia za watu wengi katika eneo hilo na kukusanyika kwa wingi wengine katika maghorofa yaliyoko katika eneo hilo kwa lengo la kushuhudia badala ya kusimuliwa jambo lililowafanya polisi kuzungushia kamba maalum kwa ajili ya kuwazuia raia kufika katika eneo hilo ambapo watu wawili mtu na mwanaye ndio walioshuhudia.

Next Post Previous Post
Bukobawadau