Bukobawadau

BIG RESULTS NOW:NI SHIDAAAA!!!

 Mikakati ya Big Results Now huenda isifanikiwe katika sekta ya elimu kwa kuwa miundombinu ya mazingira ya kufundishia haijaboreka kwa wanafunzi walimu na vyumba vya madarasa.
Pichani ni wanafunzi zaidi ya 80 wa darasa la kwanza shule ya msingi Buhororo wanaojifunzia katika chumba kimoja cha darasa la kuazima kutoka kanisa katoliki la Buhororo wilayani Ngara mkoani Kagera wakiwa na mwalimu wao
 Wanafuzi hao wenye umri wa miaka kati ya 7-9  wanakaa kwa msongamano kwa kuwa madawati ni pungufu hayatoshelezi mahitaji yao darasani huku mwalimu akifundisha bila kuwa  na vitabu vya kufundishia  na kujifunzia
 Pichani ni Baadhi ya wafanyabiashara wa nyama ya mbuzi wakiwa vichakani katika machinjio bubu zilizoko kijiji cha Rwinyana kata bugarama wilayani Ngara hivyo kufanyia kazi katika mazingira hatarishi wakihitaji machinjio ya kisasa kuboresha biashara yao
 Kufuatia hali hiyo uchunguzi uliofanywa na mwanahabari hizi unaonesha kuwa wauzaji hao wa nyama hufanya kazi zao bila kuhusisha  wagana wa mifugo ili kupima nyama hizo na kubaini kama mifugo wanayochinja  inaweza kuwa na magonjwa yanayoweza kuathiri binadamu
 Wito unaotolewa ni kwa waganga wa mifugo kuepuka kupokea rushwa ya nyama ama fedha kutoka kwa wafanya biashara wa maeneo wanakofanyia kazi bali wachukue hatua za kupima nyama za walaji huku serikali za vijiji zikiibua vipaumbele vya miradi ya kujenga machinjio ili kulinda afya za wananchi pamoja na Halmashauri ya wilaya ikusanye mapato kiuchumi.
Na Shaaban Ndyamukama
Next Post Previous Post
Bukobawadau