Bukobawadau

KWA WAKINA DADA MLIOKO KWENYE MAHUSIANO

Yamkini umeshasikia usemi usemao “mbinu bora ya kuondokana na mwanaume uliyemchoka ni kutafuta mwanaume mwingine” sawa naweza kukubaliana na wewe, lakini jiulize, je kule kuondokana na huyo unayetaka akuache kunakufanya uwe salama na mwenye furaha? Yamkini unaifuata ile methali isemayo “dawa ya moto ni moto” lakini nikutahadharishe tu kwamba sio methali zote zinatenda kazi kwenye mahusiano kama vile zilivyo, ziko nyakati kwenye mahusiano dawa ya kuzima moto siyo kuwasha moto mwingine bali ni kumwaga maji, tena ya baridi kabisa. Usije kuwa na misimamo ambayo itayafanya macho yako yasikauke machozi kwa jinsi utakavyodumu kwenye kulia kwa kuumizwa moyo kila wakati, kwasababu mwisho wa siku utajikuta umekuwa mtaalamu wa kumiliki wanaume wasiokaa. Sasa sijui wote waliopita kwako na ukawaacha uliwapenda? au ndiyo walikuwa wanapita kama wafanyakazi kwenye usahili “interview”!
Next Post Previous Post
Bukobawadau