Bukobawadau

MTANGAZAJI WA CHANNEL TEN SALUM MKAMBALA APATA AJALI

Mtangazaji wa Channel Ten, Salum Mkambala (pichani) amepata ajali ya gari ambalo alikuwa akiendesha kutoka Dar es Salaam kuelekea Morogoro. Kwa mujibu wa mmoja wa wafanyakazi wa Channel Ten ambaye ameidokeza Global Publishers.info, Mkambala alipata ajali hiyo maeneo ya Chalinze alfajiri ya leo na hali yake inaelezwa kuwa ni mahututi baada ya kuumia vibaya. Haijafahamika yuko hospitali gani kwani alikuwa peke yake kwenye gari na taarifa ilitolewa na msamaria mwema kwa simu ya Salum na baada ya hapo simu yake haipatikana tena.
source:GPL
Next Post Previous Post
Bukobawadau