Bukobawadau

NOMA NI SUAREZ ENGLAND 1-2 URUGUAY

..Mabao mawili ya Luis Suarez yanawaondoa England MAPEMA katika michuano ya kombe la dunia. 
Kwa uwezo mkubwa Suarez anatulia na mpira wakati Mchezaji  Jagielka akimnyemelea kwa nyuma
Sterling anajaribu kuondoa mpira kutoka kutoka Godin
Mshike mshike uwanjani
 Mshambuliaji wa Liverpool,  Luis Suarez ambaye mapema kabla ya michuano hii alisumbuliwa na majeraha usiku wa leo ametumia makosa ya Steven Gerrard na kutupia bao la pili kwa timu yake.




Wapenzi wa England wakitabasamu kabla mambo ayajawa magumu kwao.
Matukio mbalimbali kati ya England na Uruguay.
Shangwe za Mashabiki wa England Uwanjani
Macho ya Rooney ynaonekana yakifuatili mpira kama utatekeleza kusudio.
Mpambanaji Kipa wa Uruguay Fernando Muslera (kushoto)anadaka mpira na kuanguka chini ,mbele ya miguu ya Sturridge .
Ni mchuano  wa mataifa makubwa anaonekana  Suarez na Gerrard wakiwania mpira.


Kwa nguvu na umakini  kipa Hart anaokoa mpira ,ni shambulizi la mchezaji Cavani 


Licha ya kuwa chini bado Mchezaji wa England,Sterling anaonyesha juhudi kuumiliki mpira.
Mchezaji  Godin (kushoto) anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kuunawa mpira.
Hewani Kipa Hart anaufuata mpira
Coleen Rooney mke wa Mchezaji Wayne Rooney na Mwanae Klay wamekuwepo kushuhudia mtanange huu ndani ya uwanja wa Sao Paulo.
Jezi namba 9, ni Suarez baada ya kufunga bao .
Mchezaji Suarez anaruka juu ya bega la Phil Jagielka  na kutupia mpira wavuni
 Suarez anaunganisha mpira wavuni kwa njia ya kichwa 
 Suarez akifuatilia mateso anayompa  Joe Hart
Ni bao kwa Uruguay
Mkali Rooney akiwa amejipanga vyema na kutupia mpira wavuni. 1-1
Rooney akishangilia bao lake .
 Luis Suarez akiwaonyesha furaha baada ya kufunga bao muhimu bao la pili kwa Uruguay
Vichwa chini wanaonekana  Steven Gerrard na Phil Jagielka wakitafakari baada ya England kushindwa katika ndani ya uwanja wa Sao Paulo
Machozi yanawatoka wacheaji wa England baada ya kupoteza mchezo huu na kuondolewa katika mashindano ya Kombe lao la Dunia

Next Post Previous Post
Bukobawadau