Bukobawadau

MTAA KWA MTAA NA CAMERA YETU JULY 24,2014

 Katikati ya Mji wa Bukoba, tukielekea ndani ya Ofisi ya 'Vouchar Center',Tunakutana na Kaka Mkuu E. Nyambo akiwa falagha na Bibie Salome.akiteta jambo na Mdau Salome aka 'Mama Chui',Chui na London,chui wa mikogo,mama wa milindimo,mama Baraka,Rais wa zamani mtaa wa migeyo na Sasa ndiye Rais wa Mitaa ya Kati.
Katika hali ya usikivu akipokea maelekezo kutoka kwa Kaka Mkuu ndivyo anavyo onekana mwanamama Salome aka 'Mama Chui',Chui na London,chui wa mikogo,mama Baraka ,mama wa Milindimo,Rais wa zamani mtaa wa Migeyo na Sasa ndiye Rais wa Mitaa ya Kati.
 Ndani ya Hussein Shop hiki  ndicho kinachoendelea kurokana na punguzo la bei  katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani
 Hussein Shop ni duka la reja reja lililopo mjini hapa lenye kutoa huduma kama (super market) lenye bidhaa zenye ubora kulingana na kipato cha kila mtu.
Mambo ya usafi wa mwili ,kuna kila bidhaa kwa  ajili ya mwili,bidhaa zenye harufu nzuri na zinaweza kutumika sehemu zote za mwili ata usoni ,kulainisha ngozi yako.
Ndani ya Hussein Shop kuna bidhaa nzuri kwa kulainisha ngozi na kuifanya kuwa nyororo pia zipo bidhaa zenye kuondoa matatizo karibu yote ya ngozi.
Wateja wakiendelea kupata huduma zenye punguzo la bei .
Kijana Avith Kato katika harakati za hapa na pale.
Barabara ya Kashozi Mjini Bukoba, njia panda kuelekea Kashai.
 Ndugu Fuady kama alvyokutwa na Camera yetu, kijiweni kwa Saidi Mshamu pichani kulia.
 Kijiweni kwa Saidi Mshamu, shughuli zikiendelea.
Wadau wakibadilishana mawazo.
 Barabara ya Jamhuri kuelekea Manispaaa.
Ustaadh pichani akitambua uwepo wetu katika kuendeleza hili na lile mtaa kwa mtaa.

 Anaitwa 'Kamatria'Mzee wa 'Kisinoka' hii ni kutokana na Kipaji kikubwa alichonacho katika tasnia ya Uimbaji wa Taarabu .
 Dukani kwa Mzee Yahaya Kagambo, K.Y Enterprises wauzaji wa Vifaa vya Ujenzi.
Mkabala na Mtaa wa Haki jirani na Bank ya CRDB.Tunashuhudia Madreva wa magari haya pichani wakionyeshana ubabe.
Camera yetu ikiendelea katika pitapita mitaa ya kati mjini Bukoba.
Mdau akipata Mali Juice safi.
Vijana watanashati wa Mjini hapa ni Ndugu Eugen Kabendera na Mdau Greyson Ruge.
 Mdau maarufu kwa Jina la 'Ruge Magari' akicheck na Camera yetu mtaani
  Ingawa ubepari uliochukua sura ya uliberali,Bukobawadau BLOG tutaendelea vile vile kuakikisha tunakupatia tashira mbalimbali juu ya kinachojili na katika ubora unaostahili.
Mmoja wa wadau akifurahi mbele ya Camera yetu
 Kijana Hamza Yunusu Mgogo maarufu kama ' Katonda webala' akicheck na Camera yetu
Ukweli ni kwamba kuna Sura zimezoeleka kiasi ukikutano nazo lazima picha ihusike
Mwanalibeneke nikiendelea na Mtaa kwa Mtaa, bado naumiza kichwa hapa, mjadala ulikuwa nini kwa Kaka mkubwa na binnti yake Salome aka Chui na london .
 Pichani ni sehemu ya Wadau waliozoeleka mjini Bukoba,ukweli huu ni sawa na kile unachokiona kwenye kioo kuwa ni sura na mwili wako
 Maeneo ya Toto's moja ya Duka maarufu kwa uuzaji wa Nguo za watoto
. Toto's ni Duka la kisasa linalojishughulisha na uuzaji wa bidhaa bora na  Nguo za watoto. 
Shukrani kubwa kwako kwa kuendelea kutembele Mtandao wetu, Ombi letu kwako Jiunge nasi katika ukurasa wetu wa facebook kupitia link hii>>Bukobawadau Entertainment Media


Next Post Previous Post
Bukobawadau