Bukobawadau

UPDATES; Ajali Musoma,Kamanda wa police kasema waliofariki ni watu 39 na kujeruhiwa ni watu 79.

Takribani watu 39 wamefaraki na majeruhi zaidi ya 79 asubuhi leo baada ya mabasi ya Mwanza Coach na J4 kugongana eneo la Sabasaba huko Butiama, Mara.
 Ajali hiyo ilihusisha basi la Mwanza coach lenye namba za usajili T 736 AWJ na basi la JK express lenye namba za usajili T677 CYC. Taarifa za awali zinasema chanzo cha ajali kilitokana gari ndogo aina ya Nissan yenye namba za usajili T 332 AKK. Miili ya marehemu imehifadhiwa katika hospitali wilaya ya Musoma mkoani humo na majeruhi wanaendelea kutibiwa hospitali hapo.
Next Post Previous Post
Bukobawadau