Bukobawadau

HII KWA LEO KRISMAS:We need to see the difference

Waraka wa kwanza wa Yohana 3:18 "............ tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli". Hivi mpaka lini wewe utaendelea kusema tu kwa maneno "I love you" "na kumiss sana" "u mean a lot to me" " siwezi bila wewe" wakati hakuna hata tendo moja linalo support hayo maneno yako? Kujali hujali, msamaha hujui kuomba, shukrani huijui kabisa, kila siku unasema utajirekebisha lakini hata dalili za kurekebishika hazionekani, kila kukicha unarudia makosa yale yale ya kila siku, kama kweli unampenda mbona unashindwa kubadili hizo tabia asizozipenda ili kumruhusu akupende zaidi??. Unakuwa mzigo badala ya kuwa wa msaada kwa mpenzi wako, nakubali kabisa kwamba kusema "nakupenda" nitajirekebisha" ni maneno ya kutia moyo lakini pale yanapozidi kusemwa pasipo vidhibiti yanapoteza ladha na nguvu yake. Acha kuuza chai kwa maneno yako matupu yasiyoweza kuvunja mfupa, mpenzi wako hataki maneno matupu, anatamani kuona matendo kutoka kwako, maneno matupu hayashibishi kiu ya penzi bali maneno yenye viambatanisho vya matendo. Kama ni maneno tu hata kasuku anayo, we need to see the difference - Chris Mauki
Next Post Previous Post
Bukobawadau