Bukobawadau

MKUTANO WA CHADEMA MJINI BUKOBA LEO

Ziara ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe imeendelea kuchukua kasi mjini Bukoba leo,Mapema kabla ya Mkutano wa hadhara mbowe amezindua program ya mafunzo kwa viongozi wa chama Programu hiyo maarufu kama ‘Fast Truck Program- (FTP)’,Program ilizinduliwa kwa ajili ya mafunzo ya uzalendo kwa vijana wa chama ikiwa ni mwendelezo washughuli ambayo imekuwa ikifanywa tangu Januari mwaka huu na zoezi hili litaendelea kesho Wilayani Kyerwa Mkoani Kagera.
 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Uhuru Mjini Bukoba leo April 25,2015 pamoja na mambo mengine amewaomba wananchi wa Bukoba na Kagera kwa ujumla kuikataa CCM kwa vitendo kwa sababu imechangia kwa asilimia kubwa kuzorotesha maendeleo ya wanakagera
Mbowe amesema;"wakati wa mabadiliko ni sasa,tuungane pamoja kukamata dola Oktoba mwaka huu"
 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, akihutubia mamia ya wakazi wa Mji wa Bukoba mkoani Kagera, katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa juzi
 Mheshimiwa Mbowe ameongozana na Viongozi waandamizi wa Kitaifa wakiwemo watia nia wa ubunge kutoka majimbo mbalimbali ya uchaguzi mkoani Kagera.
Mtia nia Roderick Lutembeka na 'Kifuba' Wilfred Lwakatare wamepata fursa ya kuhutubia katika mkutano huo pamoja na aliyewahi kuwa kada mahili wa ccm nchini Dr. Azavery Lwaitama ambaye sasa ni muhadhiri wa chuo kikuu kimoja kilichopo mkoani Kagera (JOKUCO)
 Umati wa wananchi wakimsikiliza Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe
 Sehemu ya wakazi wa mji wa Bukoba waliohudhuria mkutano huo
 Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha  JOKUCO, Dk Azavery Lwaitama akiwahutubia wananchi mjini Bukoba leo katika mkutano wa hadhara wa Chadema.
 Sehemu ya wananchi wakimshangilia Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Muganyizi Lwakatare
 Wilfred Muganyizi Lwakatare( Kifuba) akiendelea kuwahutubia wakazi wa mji wa Bukoba
 Mkurugenzi wa ulinzi na Usalama @Chademataifa Wilfred Lwakatare pamoja na mambo mengine amewaelezea wakazi wa mji wa bukoba nia yake ya kugombea jimbo la Bukoba Mjini

 Mkutano ukiendelea sehemu ya walihudhuria wakiendelea kusikiliza kwa umakini.
 Mratibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Ziwa Victoroia, Renatus Bujiku, akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa mjini Bukoba mkoani Kagera
 Wananchi wakionyesha Ishara ya vidole viwili juu na kuimba 'Peoples Power'
Meza kuu wakisikiliza hoja mbalimbali
 Wakati mkutano ukiendelea.
 Taswira mbalimbali kutoka Uwanja wa Uhuru Mjini Bukoba leo April 25,215
 Bw. Roderik Lutembeka katika hali ya usivu 
 Sehemu ya viongozi waandamizi wa Chadema
Mbowe ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) linaloundwa na vyama vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD, kesho ataendelea na ziara yake Mkoani Kagera Wakati viongozi wengine wa Kitaifa nao wametawanyika katika kanda mbalimbali za kichama, wakiendelea kutoa mafunzo kwa viongozi wao wa serikali za mitaa, ambayo yalizinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam wiki iliyopita.
Mbowe anahitimisha Mkutano wa hadhara uliofanyika leo katika Uwanja wa Uhuru Bukoba
kwa kuwataka wananchi kukunja ngumi ili waagane kwa salamu yao

 Ishara ya Nguvu ya Umma (People's Power),kwa matukio ya picha zaidi ungana nasi katika ukurasa wetu wa facebook kupitia link hii>BUKOBAWADAU MEDIA



Next Post Previous Post
Bukobawadau