Bukobawadau

MASHINDANO YA UMISETA MKOANI KAGERA YAZINDULIWA RASMI



Mkoa wa Kagera umeanza rasmi mashindano ya UMISETA yanayowashirikisha wanafunzi wa shule za sekondari kutoka katika Halmashauri zote  za Wilaya na Manispaa ya Bukoba katika mkoa wa Kagera.
Mashindano hayo yalifunguliwa jana tarehe 21/05/2015 na Afisa Elimu Mkoa wa Kagera Bw. Aloyce Kamamba katika viwanja vya Chuo cha ualimu Katoke Wilayani Muleba.
Akifungua mashindano hayo Bw. Kamamba aliwaasa wanafunzi wanamichezo ambao wamejumuika katika chuo cha Katoke  kwa kushindana katika michezo mbalimbali kutumia fursa hiyo kuonesha vipaji vyao kwani kwa sasa michezo ni ajira.
Pia Bw. Kamamba aliwaasa wanamichezo hao kuhakikisha wanacheza na kushindana kirafiki bila kucheza kwa kuumizana na kuhakikisha waamuzi wanachezesha bila upendeleo.
Walimu wanaohusika kuchezesha na kusimamia michezo hiyo katika mashindano hayo ya UMISETA mkoa pia nao walihaswa kuhakikisha wanasimamia nidhamu na kuhakikisha wanachagua wachezaji wazuri ambao watakwenda kushindana na kuonyesha vipaji vyao pia kuleta makombe ya ushindi.
Aidha, Afisa Michezo wa Mkoa wa Kagera Bw. Kepha Elias akitoa ratiba ya mashindo alisema kuwa mara baada ya mashindano hayo kukamilika ngazi ya mkoa timu zitakazokuwa zimechaguliwa zitapiga Kambi kwa siku tatu ili kufanya maadnalizi ya kushiriki mashindano ya Kanda.
 Bw. Kepha alisema kuwa mshindano ya Kanda yatafanyika mkoani Geita ambapo mara baada ya hapo wachezaji watakaokuwa wamechaguliwa wataelekea mkoani Mwanza kushiriki mashindano ya UMISETA kitaifa mkoani humo.
Next Post Previous Post
Bukobawadau