Bukobawadau

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI- KIKAO CHA KAMATI KUU CHADEMA



Taarifa inatolewa kwa vyombo vya habari kuwa kuwa Kamati Kuu ya Chama, chini ya Mwenyekiti wake Freeman Mbowe, itakutana Mei 3-4, katika kikao chake cha kawaida kwa mujibu wa Katiba ya Chama.
Katika kikao hicho cha siku mbili kitakachofanyika jijini Dar es Salaam, pamoja na masuala mengine ya kitaifa kuhusu hali ya kisiasa nchini kwa ujumla na mengine mahsusi yanayohusu uendeshaji wa chama, KK itapokea taarifa, kujadili na kufanya maamuzi kuhusu;
1.     Maandalizi ya Chama kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
2.     Taarifa ya ziara ya mafunzo kwa timu za kampeni, viongozi wa serikali za mitaa na chama, kukiandaa chama kushinda dola na kuongoza serikali baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
3.     Taarifa za utendaji wa chama kupitia kanda zote 10, Tanganyika na Zanzibar.
4.     Taarifa ya maendeleo ya mikakati ya kushiriki uchaguzi mkuu kwa kushirikiana na vyama 4 vinavyounda UKAWA.
5.     Taarifa za mwenendo wa shughuli ya uandikishaji wa wapiga kura (upya) katika daftari la kudumu kwa teknolojia ya Biometric Voters Registration (BVR) na hatma ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Imetolewa leo Jumamosi, Mei 2, 2015 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara a Habari na Mawasiliano- CHADEMA
Next Post Previous Post
Bukobawadau