Bukobawadau

Mdahalo wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere wataka amani, wapinga rushwa Uchaguzi Mkuu Oktoba 2015.

 Mtoa mada Awadh Ali Said, akitoa mada kuhusu muungano na umuhimu wa kuzingatia misingi ya amani katika mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere ambao ulifanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam leo.
 Mtoa mada Dk. Humphrey Polepole akitoa mada kuhusu kuzingatia misingi ya amani na umoja wa taifa letu kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 2015.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku akitoa majumuisho ya jumla juu ya dhima ya mdahalo huo, ambapo aliwataka watanzania kuendelea kupiga vita rushwa na kusisitiza kutowachagua watoa rushwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku (kushoto), akiteta jambo na watoa mada katika kongamano hilo, Jaji mstaafu Joseph Warioba na Dk.Humphrey Polepole (katikati)
 Jaji mstaafu Joseph Warioba, akimuonesha Dk. Humphrey Polepole ujumbe mfupi aliotumiwa kwenye simu yake .
Jaji mstaafu Joseph Warioba akisalimiana na washiriki wa mdahalo huo baada ya kumalizika. Mdahalo huo uliorushwa moja kwa moja na Kituo cha Televisheni cha ITV.
 Wadau mbalimbali wakiwa kwenye mdahalo huo.
 Jaji mstaafu Joseph Warioba (kulia), akiwaaga washiriki wa mdahalo huo. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii. com-simu namba 0712-727062)


Next Post Previous Post
Bukobawadau