Bukobawadau

RC DAR ES SALAAM NA KOREA KUSINI WAWEKA JIWE LA MSINGI LA HOSPITALI YA CHANIKA MANISPAA YA ILALA


 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kulia) na Makamu wa Rais wa Shirika la Koica la nchini Korea Kusini, Taemyon Kwon, wakiweka tofali kwa pamoja kuashiria uweka wa jiwe la msingi la Hospitali ya Chanika iliyopo Manispaa ya Ilala, inayojengwa kwa ufadhili wa nchi hiyo Dar es Salaam jana. Ujenzi huo hadi kukamilika utagharimu sh. bilioni 8.8  za kitanzania.
Hutuba na taarifa ya mradi huo zilisomwa.



 Balozi wa Korea nchini Geum-young Song (katikati), akizungumza katika hafla hiyo.
Wananchi wa Chanika wakiwa kwenye hafla hiyo ya kuweka jiwe la msingi la Hospitali yao.
Diwani wa Kata ya Chanika, Mr Massaburi akitoa neno la Shukurani kwa RC Makonda, Serikali pamoja na Serikali ya Korea kwa ujenzi wa Hospitali hiyo.


Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Mr Isaya (kulia), Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Magembe, Mganga Mkuu wa Manispaa ya Ilala, Victriana Ludovic na Meneja wa Mradi wa ujenzi wa Hospitali hiyo Mr Kim wakiweka jiwe la msingi la Hospitali hiyo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Chanika wakiwa kwenye hafla hiyo.
Meneja wa Mradi huo, Mr Kim akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na ujembe wake ramani ya majengo ya Hospitali hiyo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Chanika wakitoa burudani katika hafla hiyo.
Wasanii wakitoa burudani katika hafla hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Manispaa ya Ilala na Korea Kusini

Na Dotto Mwaibale

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda na balozi wa Korea nchini Geum-young Song wameweka jiwe la msingi la Hospitali ya Chanika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam ambapaaaaaaaaaao itakapo kamilika itakuwa na uwezo wa kuhudumia wananchi 4000.

Akizungumza katika hafla ya kuweka jiwe hilo la msingi Chanika jijini Dar es Salaam jana, Makonda aliishukuru serikali ya Korea kwa msaada wa ujenzi wa Hospitali hiyo ambayo itawasaidia wananchi wa Chanika na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Amana.

"Tunawashukuru hawa ndugu zetu wa Korea Kusini kwa msaada wa kutujengea Hospitali hii nawaombeni wananchi kuitunza ili kila mtakapokuwa mnafika kutibiwa tuwakumbuke wakorea" alisema Makonda.

Mganga Mkuu wa Manispaa ya Ilala, Victorina Ludovic alisema ujenzi wa Hospitali hiyo utasaidia kusogeza huduma muhimu karibu na wananchi wapatao 398,882 kutoka maeneo ya Chanika, Msongola, Zingiziwa na Majohe hivyo kupunguza muda na gharama ambazo wananchi wamekuwa wakitumia kufuata huduma hizo umbali wa kilometa 30 kwenda hospitali ya Amana ya Rufaa.

Ludovic alisema ujenzi wa mradi huo hadi utakapokamilika  utagharimu dola la milioni 4 sawa na sh.bilioni 8.8 za kitanzania.

Balozi  wa Korea nchini , Geum-young Song amesema wakorea hawafurahishwi wanapoona mama na mtoto wanapoteza maisha wakati wa kujifungua nchini Tanzania.

"Nchi yetu kupitia shirika la Koica imeamua kujitolea kujenga hospitali hii ili kuwasaidia wananchi wa Tanzania kupata huduma bora ya afya ya mama na mtoto wakati wa kujifungua kwani hatupendi kuona wanapoteza maisha wakati wa kujifungua" alisema Young Song.

Balozi huyo aliipongeza serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na nchi ya Korea katika shughuli mbalimbali jambo linaloimarisha uhusiano baina ya wananchi wa nchi hizo.

Next Post Previous Post
Bukobawadau