Bukobawadau

WABUNGE WENGI WAIBARIKI BAJETI WIZARA YA AFYA

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalim akihitimisha majumuisho ya makadirio ya Bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017, bungeni Dodoma usiku huu.
 Waziri Ummy Mwalim akipanga vizuri nyaraka tayari kuhitimisha majadiliano ya makadirio ya bajeti ya wizara hiyo.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Viongozi wa wizara hiyo wakifuatilia majadiliano ya wabunge kuhusu bajeti hiyo.
 Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Hamis Kigwangallah akijibu moja ya hoja za wabunge.
 Mbunge wa Viti Maalum, Sophia Mwakagenda (Chadema), Mkoa wa Mbeya, akichangia hoja wakati wa makadilio ya Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa iliyopitishwa bungeni Dodoma
 Naibu Waziri wa Afya, Hamisi Kigwangala akisalimiana na wanafunzi wanaosomea utabibu katika Chuo Kikuu cha Dodoma waliozuru bunge mjini Dodoma

 Mbunge wa Viti Maalum, Halima Bulembo akichangia wakati wa majadiliano ya Bajeti ya wizara hiyo
 Mbunge akiingia bungeni Dodoma leo
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage (kulia) akijadiliana jambo na Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Saed Kubenea (Chadema), kushoto, pamoja na Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini, Anthony Komu (Chadema), walipokuwa wakiingia bungeni Dodoma
 Mbunge wa Jimbo la Ulanga, Goodluck Mlinga akitaniana na wanahabari (hawapo pichani) alipokuwa akiingia bungeni Dodoma. Kulia ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Hussein Ali Mwinyi.
 Wabunge wakiingia bungeni Dodoma

 Mbunge wa Segerea, akiichangia hoja wakati wa wizara ya Afya. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum,  Bupe Mwakang'ata.
 Mbunge wa Donge, Sadifa (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju (kulia). Kushoto ni Mnadhimu Mkuu wa Bunge wa Serikali, Jenista Mhagama.




 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina (wa pili kulia) akizungumza na wawakilishi wa wafugaji wa mikoa ya Kanda ya Ziwa na Magharibi waliofika bungeni Dodoma, kukutana na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba kujadiliana jinsi ya kutatua tatizo la malisho.







Next Post Previous Post
Bukobawadau