Bukobawadau

TKIFO CHA JOSEPH SANGA WA TANZANIA DAIMA!

TANZIA.Mpiga picha mkongwe wa habari nchini ambaye amewahi kuwa mpiga picha mkuu wa gazeti la Tanzania Daima, Joseph Senga (pichani) amefariki dunia. Senga ndiye aliyepiga picha ya Daudi Mwangosi wakati anauawa na askari Polisi katikat Mji Mdogo wa Nyololo, mkoani Iringa. Mungu ampumzishe kwa amani.!!
 Ameandika Dotto Bulendu wa Star Tv;Simanzi,siku moja baada ya mahakama kuu kanda ya Iringa kumfunga miaka kumi na mitano askari ya aliyemuua Daudi Mwangosi,tasnia ya habari yapata pigo,mpiga picha wa gazeti la Tanzania Daima,aliyepiga picha za tukio la mauaji ya Daudi ya Mwangosi,SHUJAA JOSEPH SENGA,amefariki dunia usiku huu.
Senga amefia nchini India alikopelekwa kwa matibabu ya ugonjwa wa Moyo.
Bila Joseph Senga,shujaa aliyehatarisha maisha yake,akasimama bila woga,akapiga picha akiwa katikati ya msitu wa askari polisi wenye silaha,huku anga ikiwa imegubikwa na moshi wa mabomu ya machozi,milio ya risasi ikisikika,na kuzitunza,zikasaidia kufichua mauaji ya Mwangosi,leo hii asingekuwa Senga,nadhani kusingekuwa na kesi na mwisho hukumu dhidi ya aliyemuua Mwangosi.Nakulilia Senga..
Senga,Senga,Senga,Senga,umekwenda,Mungu aliamua akuweke hai mpaka hukumu itoke na mwisho amekuchukua,Senga umekwenda wadogo zako katika tasnia tukiwa na hamu ya kujifunza kutoka kwako.
Senga,Senga,kamsalimie Daudi Mwangosi,mwabie aliyemuua nae kahukumiwa jela miaka 15,kamwambie mazingira ya waandishi wa habari bado magumu.
Nenda Senga,picha zako zinabaki kuwa rejea ya mafunzo ya uandishi wa habari katika mazingira hatarishi.
Next Post Previous Post
Bukobawadau