Bukobawadau

PATA SIMULIZI LA LEO

Baba mmoja alikuwa akila chakula kwa furaha na mke wake ambaye alikuwa siku za mwisho akijitazamia kabla ya kujifungua mtoto wao wa kwanza.
Mara mama akaanza kulalalamika maumivu ya kichwa na baba akaita gari na wakiwa njiani kuelekea hospotali yule mama akafariki.
walipofika hospitali baba akaomba mama afanyiwe upasuaji wa haraka ili waone kama mtoto aliyekuwa tumboni angeweza kupona.
Baada ya upasuaji wa haraka mtoto alitoka akiwa mzima na madaktari wakiwa wanashangaa baba aliendelea kuomba kwa Mungu akisema;
" Eeh Mungu kama umeweza kumwokoa mtoto huyu naamini pia waweza kuurejesha Afya ya mama yake
Ikiwa ni mapenzi yako naomba mke wangu kipenzi apone na kumshuhudia mwanae aliyemgojea kwa siku nyingi na hamu tele.
Ninaomba nikiamini kuwa wewe ni Mungu wa miujiza na mwenye huruma kwa sisi watoto wako AMEN"
Jopo la madaktari waliokuwa wakimsaidia yule mama wakaanza kushangaa kwa mbali mama mapigo ya moyo yakaanza kurudi na baada ya jitihada mama alipona na kila mtu mle ndani aliushangaa ule muujiza huku wakiwa na mshtuko wakamshukuru Mungu.
Sasa naomba nawe usikie maneno haya kwa makini!!!!!!
*Mungu akupe wepesi, amani na furaha kwa kila tatizo litakaloyasibu maisha yako
*Kamwe usichoke kumwomba Mungu hata kwa jambo unaloliona machoni mwako haliwezekani, kwani kwa Mungu hakuna linaloshindikana
*Kuanzia leo katika kila jambo uliloliona kuwa gumu kwako litakuja kuwa rahisi na liwezekanalo
*Kwa kila jambo lililokuwa likichelewa katika maisha yako kuanzia sasa litaanza kwenda haraka nawe utashangaa ukuu wa Mungu.
*Utafurahia mafanikio ya kila jambo na ukishuhudia miujiza katika maisha tyako.
Comment AMEN na kisha share kama unaamini katika miujiza ya Mungu kwenye maisha yako.
Next Post Previous Post
Bukobawadau