Bukobawadau

SHIDA KUBWA YA MAJI WILAYANI KARAGWE!!

Ukweli ni kwamba ukiwa nje ya wilaya hii ya Karagwe hutawaza kwamba kuna uwezekano wa kuwepo tatizo la maji la kiasi hiki katika maeneo mengi na Mji wa Kayanga ambao ndio makao makuu ya Wilaya yenye majimbo mawili makubwa ya Karagwe na Kyerwa
 Foleni kubwa ya wananchi wakati wakisubilia huduma ya maji maeneo ya Omulushaka Karagwe
 Pichani wanaonekana Wakazi wa kijiji cha Kiyanga  Wilayani Karagwe  Mkoani Kagera wakichota maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kutoka katika shimo lilochimbwa bondeni ,na hiki ndicho chanzo kikubwa wanachokitegemea pamoja na kwamba maji hayo ambayo kwa kiasi kikubwa hutegemea kunyesha kwa mvua sio salama kwa binadamu,wakiongea na mwanalibeneke wetu Wakazi hao wamesema kwa muda mrefu wamekuwa wakitumia maji hayo hayo.
Kadhia hii ya maji ni alama mbaya sana kwa wazawa wote wa Karagwe  waishio ndani na nje ya Wilaya ya hii  pia ni aibu na alama kubwa ya usaliti wa wawakilishi wao wote wa vipindi mbalimbali!!
Hakika ni lazima zitumike nguvu za ziada kuwaokoa wananchi  hawa wanaokatiza usingizi kila siku kwenda kupanga foleni ya maji katikati vyanzo mbalimbali.
Credit Photo:@Mc Baraka

Next Post Previous Post
Bukobawadau