Bukobawadau

HUKO KANYIGO MAELFU WAMZIKA BI ESTHER RWEGASIRA


Hivi ndivyo ilivyokuwa Safari ya Mwisho ya Maisha ya Bi Esther Rwegasira aliyekuwa Mke wa Marehemu Balozi Joseph Rwegasira aliyekuwa Mwenyekiti wa vyama vya wafanyakazi JUWATA, Mkuu wa Mkoa wa kwanza wa Pwani na baadaye balozi wa Tanzania nchini Zambia halafu akawa Waziri wa viwanda na Biashara, na baadaye waziri wa Kazi na mwisho Waziri wa mambo ya nchi za nje,na Mbunge wa Nkenge mpaka mwaka 2000.
Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Lt.Col.Denis Filangali Mwila akisalimiana na wafiwa mara alipofika msibani hapo kumwakilisha mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa ambeya ni Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Lt.Col.Denis Filangali Mwila pichani kulia akitoa mkono wa pole kwa wafiwa alipofika kushiriki Shughuli ya maziko ya Marehemu Bi Esther Rwegasira yaliyofanyika siku ya Ijumaa nyumbani kwake Kijijini Bukombe Kanyigo

Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera, Costansia Buhiye ,bi Halima katibu wa Wazazi Wilaya Missenyi na wa mwisho kulia ni Mama Mbae katibu wa CCM wilaya ya Missenyi

Wanaonekana Mamia ya Waombolezaji wakiwa na nyuso zenye huzuni wakati wa shughuli ya Ibada ya Mazisho ya Marehemu Bi Esther Rwegasira .
Julius (Tiba) Rwegasira akiwa amebeba picha ya Marehemu Mama yake mpendwa

Hakika ni Simanzi kubwa kwa wanafamilia na waombolezaji kwa ujumla kufuatia msiba huu mkubwa
Muonekano wa Jeneza lenye mwili wa Marehemu Bi Esther Rwegasira
Joanitha na Pamela ambao ni watoto wa kike wa marehemu wakiwa na simanzi kubwa.
Wakati mwili wa Marehemu ukitolewa ndani.
Anaitwa Lutta mtoto wa mwisho wa Marehemu Bi Esther Rwegasira akiweka Msalaba kwenye Jeneza muda mchache kabla ya Ibada maalum kuanza
Bi Juliana Mero mkazi wa Manispaa ya Mji Bukoba ameweza kushiriki shughuli ya maziko ya rafiki yake mpendwa.

Taswira mbalimbali waombolezaji wakiendelea kufuatilia kinachojiri msibani hapa.
Waumini wa Kikatoliki wakiendelea kushiriki Ibada ya Mazishi ya Marehemu Mpendwa wetu Esther Rwegasira
Shughuli ya Maziko ya Marehemu Bi Esther Rwegasira yaliyofanyika Nyumbani kwake Kijijini Bugombe-Kanyigo Wilayani Missenyi yaliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera na Viongozi wa Vyama na Serikali.

Mamia ya waombolezaji wakiendelea kushiriki Ibada ya Maziko
Ibada ya maziko ikiendelea
Pichani katikati ni Mr.Shuli Mrengo yeye ni mkwe katika familia hii


Umati wa wananchi wa Kiijiji cha Kanyigo na maeneo mengine ya jirani wakiwa wamejitokeza kwa wingi kuuaga na kuuzika mwili wa Mpendwa wao.

Pichani anaonekani ndugu Essau Kayungi
Umati wa Waombolezaji wakiwa na nyuso zenye uzuni

Moja ya familia iliyoguswa na msiba huu mkubwa ni Mfamilia ya Marehemu Mzee Njunwa wa Kanyigo, pichani kushoto anaonekana Bi Jovitha Njunwa katika hali ya majonzi

Photo Credit @ Mc Baraka


Kushoto pichani anaonekana Mzee Joseph Masabala na kulia kabisa ni Mzee Elias Mashashi


Umati wa maombolezaji wakiendelea na Ibada maalum ya Mazishi ya Bi Esther Rwegasira



Wanakwaya wakiendelea kuimba moja ya nyimbo za kumtukuza Mungu wakati wa shughuli ya mazishi hayo iliyofanyika tarehe 2,9,2016 huko Kijijini Bugombe Kanyigo.

Bw. Hafidh (Nkurukumbi) na Bw. Haruna Goronga pichani wakiwa mamehudhuria maziko hayo

Shughuli ya Ibada ya mazishi hayo ikiongozwa na Fr.Medericus Kyaruzi wa Parokia ya Mugana.

Wanafamilia wakitoa heshima za mwisho kwa Bi Esther Rwegasira

Wanafamilia wakiendelea kushiriki zoezi la kutoa heshima za mwisho kwa mpendwa wao


Mtoto wa Marehemu Bi Esther Rwegasira,pichani ni Jovitha Rwegasira akitoa heshima zake za mwisho kwa mpendwa mama Yake.

Dada Joanitha akitoa heshima zake za mwisho

Watu wakishindwa kabisa kujizuia kutoa machozi ya huzuni wakati wa kutoa heshima zao za mwisho kuaga mwili wa Marehemu Bi Esther Kyaruzi

Poleni sana wote mliofika na msiba huu





Zoezi la kutoa heshima za mwisho likiwa badao linaendelea



Utaratibu wa kutoa heshima za mwisho ukiendelea





Baadhi ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali waliohudhuria mazishi hayo wakishirikiana na wanafamilia katika kutoa heshima za mwisho kumuaga mpendwa wao






Pole Sana Dada Pamela kwa kuondokewa na mama yako mpendwa

Wanafamilia na waombolezaji kwa pamoja wakiendelea kutoa heshima zao za mwisho



Fr.Medericus Kyaruzi wa Parokia ya Mugana akinyunyuzia maji ya baraka kwenye Jeneza lenye mwili wa Marehemu Bi Esther Kyaruzi

Fr. Rwiza Matias akiweka maji ya Uzima kwenye Jeneza lenye mwili wa Marehemu Bi Esther Rwegasira

Sehemu ya wadau walioshindikiza mwili wa Marehemu kutoka Jijini Dar es Salaam


Watoto wa Marehemu wakishiriki zoezi la kuweka Udongo

Utaratibu wa kuweka Udongo kwenye kaburi


Eneo la kaburini Shughuli ya Maziko ya Marehemu Bi Esther ikiendelea jioni ya Jana Ijumaa Sep 2,1015

Mr. Shuli Mrengo akiendelea kushiriki mazishi ya mama mkwe wake Marehemu Bi Esther Rwegasira.

Padre wakati wa kusimika msalaba kwenye Kaburi la Mpendwa wetu Ma Esther Rwegasira


Utaratibu wa kuweka mashada ya Maua kwenye Kaburi la Marehemu Bi Esther Rwegasira

Rutta na Tiba ambao ndio watoto wa kiume wa Marehemu Bi Esther Rwegasira wakiweka shada la maua.

Watoto wa kuzaliwa na Marehemu Bi Esther Rwegasira wakati wa utambulisho

Waonekana baadhi ya wanafamilia pichani

Kutoka Kijijini Bugabo pichani ni Kaka wa Marehemu Bi Esther Rwegasira

Kijana Julius (Tiba) Rwegasira akisoma wasifu wa Marehemu Mama yake mzazi Bi Esther Rwegasira

Salaam za rambirambi kutoka kwa Diwani wa Kata ya Kanyigo

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Missenye Mh. Tegamaisha akitoa salaa za rambirambi

Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Lt.Col.Denis Filangali Mwila akitoa Salaam za rambirambi kwa niaba yake na kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera

Diwani wa Kata Kashenye(Omulangira)Adeodatus Rugaibula ameweza kushiriki kikamilifu shughuli hii ya maziko iliyofanyika Kijijini Bugombe-Kanyiko Wilayani Missenyi na kuhudhuriwa na maelfu ya waombolezaji

Dr. Iganga Gerrad msemaji wa familia ya Marehemu Bi Esther Rwegasira wakati akitoa neno

Bi Jovitha pichani katikati akijadili jambo wao wanasema 'OKUTEGEKA' na watoto wa Marehemu Tiba na Luta.

Wanaonekana Watoto wa Marehemu Bi Esther Rwegasira katika wimbi kubwa la mawazo, kutoka kushoto pichani ni Luta (Joel),Tiba (Julius) na Joanitha.

Wanaonekana wadau pichani muda


Mdau Kelvin, rafiki wa familia ya Marehemu Bi Esther Rwegasiea

Ikafika fursa ya waombolezaji kupata huduma ya Chakula

Picha ya leo ni Mmoja wa Majah tulioweza kukutana nao katika shughuli ya maziko haya

Huduma safi ya Chakula ikiendelea kwa watu wote waliweza kushiriki shughuli ya maziko hayo

Muonekano wa menu husika.

Kikubwa hapa ni ishu ya mpangilio mzuri wa chakula,hakika jamaa walionekana kujipanga vyema.

Maeneo ya banda ya Mifugo tunakutana na Vijana Ma home Boy wa Kijijini hapa, tunavutiwa na maongezi yao wanavyoendelea 'Kuganyila' na 'Kutensa' kwa namna ya pekee juu ya wema wa Mama huyu Marehemu Ma Esther.

Waombolezaji wakiendelea kupata mulo, hii ni kuanzia saa tano asubuhi mpaka nane mchane kabla ya kuanza kwa Ibada maalum ya maziko ya Mama yetu mpendwa Marehemu Bi Esther Rwagasira




Baadhi ya wanafamilia wakati wa huduma ya chakula

Huduma ya Msosi ikiendelea.

Sehemu ya wanafamilia wakihakikisha kila kitu kinaenda kama kilivyopangwa



Mpangilio mzuri na huduma safi ya Chakula ikiendelea haki bin Sawa kwa watu wote




Muendelezo wa matukio wadau wakiendelea kupata huduma ya Chakula


Nyumbani kwa Marehemu Bi Esther Rwegasira , yalipofanyika maziko yake .





Kufikia hapa BUKOBAWADAU tunakukumbusha kuwa Usisite kutembelea ukurasa wetu wa facebook kwa matukio ya picha zaidi ya 400 na matukio mengine yanayojiri popote pale jiunge nasi kwa ku like' LINK hii BUKOBAWADAU MEDIA

Pichani Bi Esther Rwegasira akitoa sadaka yake kwa mzee Baitromayo Tibawa mkazi wa Kijiji cha Bugombe Kanyigo Wilayani Missenyi,mzee huyu inaaminika kuwa na Umri wa Miaka 105 ,Mzee huyo bado bado ana kumbukumbu ya mengi na yupo imara katiki kufanya shughuli zake kwa kujiongoza mwenyewe.

Naye Mh. Amoody Migeyo Diwani wa Bugandika aliweza kupata fursa ya kutoa Chochote kwa mzee huyo Kikongwe ,Mzee Baitromayo Tibawa mkazi wa Kijiji cha Bugombe Kanyigo mwenye uwezo wa hujiliwaza kwa chupa mbili au tatu za 'Kalinya'

Salaam za rambirambi kutoka kwa Uongozi wa KADEA


Kijana Feruz aliyeweza kushiriki shughuli ya maziko haya

Ni Uzuni na majonzi vikitawala moyoni mwa kila mtu kwa kumpoteza Mama yetu, mlezi wetu, Bibi yet mpendwa Marehemu Bi Esther Rwegasira

Muonekano wa Sehemu ya maegesho

Kupitia Bukobawadau Media tunakufikishia taswira kamili yaliyojiri msibani hapo


Waombolezaji  wakiendelea kutoa mkono wa pole kwa wafiwa.


Kutoka Mjini Bukoba pichani ni Kijana Martin akiwafariji wafiwa kufuatia msiba huu mkubwa wa Mama yetu mpendwa Marehemu Bi Esther Rwegasira


Mdau Martin akiwafariji wafiwa kufuatia msiba huu mkubwa wa Mama yetu mpendwa Bi Esther Rwegasira

BUKOBAWADAU MEDIA tunapenda kukufahamisha kuwa tunao uwezo wa kukupa nafasi ya matangazo katika mtandao wetu pia kwa taarifa au shughuli yotote ili kufikia idadi ya watu unaotaka kokote dunia waweza kuwasiliana nasi kupitia namba +255 784 505045,0754 505043,0715 505043 .




Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera, Costansia Buhiye




Matukio ya picha yaliyojiri msibani hapo

Aliyekuwa mme wa Marehemu Bi Esther , pichani ni Marehemu Balozi Joseph Rwegasira enzi za uhai wake
Bukobawadau tunaendelea kutoa pole kwa wote waliofikwa na msiba huu pia tunakukumbusha kuwa Usisite kutembelea ukurasa wetu wa facebook kwa matukio ya picha zaidi ya 400 na matukio mengine yanayojiri popote pale jiunge nasi kwa ku like' LINK hii BUKOBAWADAU MEDIA



Next Post Previous Post
Bukobawadau