Bukobawadau

#TETEMEKOBUKOBA:WAZIRI MKUU KASSIMU MAJALIWA AONGOZA MAMIA KUAGA MIILI YA MAREHEMU 16 WALIOKUMBWA NA TETEMEKO LA ARDHI!!

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ameongoza mamia ya wananchi wa Mkoa wa Kagera waliofurika uwanjani Kaitaba kuiaga miili ya wapendwa wao waliofariki wakati mkoa huo ulipopatwa na janga la tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, 2016 saa 9:00 alasiri na kusababisha vifo vya wananchi 16, kujeruhi 253 pia na kusababisha nyumba 840 kuanguka na nyumba 1,264 kupata nyufa.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwapa pole wananchi wa Mkoa wa Kagera kwaniaba ya Serikali na kusema kuwa Serikali inafanya juhudi zote za kutuma wataalam kuja Mkoani Kagera kuangalia kama tetemeko la ardhi litarudia tena au dalili za lini linaweza kutokea tena ili kutoa elimu kwa wananchi jinsi ya kujikinga na tetemeko hilo pindi linapotokea tena. 
Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa alisema tayari ofisi yake imetuma Wataalamu wa kitengo cha maafa ili kufika Mkoani Kagera kufanya tathimini ya kina na ya haraka wakishirikiana na kamati ya maafa ya mkoa ili kubaini ni sehemu gani zinazohitaji huduma au msaada wa haraka ambapo janga la tetemeko limesababisha madhara makubwa.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Kijuu akitoa taarifa jinsi tetemeko hilo lilivyotokea na madhara yaliyosababishwa na tetemeko hilo alimweleza Waziri Mkuu Kassim majaliwa kuwa tetemeko hilo lilitokea majira ya saa 9:00 alasiri, aidha, tetemeko hilo lilikadiriwa kuwa na ukubwa 5.7 katika vipimo vya Richter na lilisababisha madhara makubwa katika mkoa mzima.
Mhe. Kijuu alimweleza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuwa tetemeko hilo lilisababisha vifo vya wananchi 16, majeruhi waliolazwa katika Hospitali mbalimbali zilizoko kwenye mkoa wa Kagera ni 170, Majeruhi waliotibiwa na kuruhiusiwa ni 83 na jumla ya majeruhi wote ni 253. Aidha nyumba za makazi zilizoanguka ni 840, nyumba zilizopata nyufa ni 1,264 na majengo ya taasisi yaliyoripotiwa kuanguka ama kupata nyufa ni 44.
Aidha, Mkuu wa Mkoa alimweleza Mhe, Majaliwa kuwa mara baada ya tetemeko hilo kutokea uongozi wa mkoa ulichukua hatua za haraka kwa kuokoa wananchi na kuwapeleka hospitali mbalimbali kwa ajili ya matibabu. Pili, baadhi ya wananchi wenye nyumaba zilizoathirika walipatiwa makazi ya muda na kuwahamasisha kusaidiana wao kwa wao kupeana hifadhi. Mwisho Mkoa unaendelea na tathimini ya athari na hasara zilizosababishwa na tetemeko hilo.

Agizo la Waziri Mkuu, Mkoa chini ya Mwenyekiti wa kamati ya Maafa ya mkoa ambaye ni Mkuu wa Mkoa pia na Maafisa kutoka kitengo cha Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu waendelee kufanya tathmini ya kina ya kubaini athari na hasara za tetemeko hasa kwa kuanza na sehemu zinazohitaji huduma ya haraka kama shule mbili za Sekondari za Ihungo na Nyakato ili Serikali iweze kusaidia mara baada ya kupata tathimini ya hali halisi ya maafa.
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kuwasiili Mkoani Kagera majira ya saa 7:00 mchana aliwatembelea majeruhi waliojeruhiwa wakati wa tetemeko hilo ambao bado wamelazwa katika Haspitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera, pia alitembelea shule za Sekondari za Nyakato na Ihungo ambako madhara yalitokea makubwa na kupelekea wanafunzi kukosa sehemu za kulala baada ya mabweni yao kubomolewa na tetemeko.
 Vile vile Mhe Majaliwa alishuhudia maiti 14 na kutoa heshima zake za mwisho kwa marehemu katika uwanja wa Kaitaba ambapo marehemu hao waliombewa dua na sala kutoka kwa viongozi wa dini Mkoani Kagera . Pia Mhe. Majaliwa aliwapa pole wafiwa na kuzungumza na wananchi waliokusanyika uwanjani hapo kwa kuwapa salaam za Serikali.
Credit kwake Mwanahali Sylvester Raphael wa Ofisi ya RC Kagera
 Mamia ya watu waliojitokeza Uwanjani Kaitaba Kuaga miili ya Wapendwa wao
 Mzee Al Haji Abbakari Galiatano akiteta na rafiki yake William Ruta
Mzee Abdulziad Kashide akiwasili Uwanjani Kaitaba kushiriki zoezi la kuaga Miili ya marehemu 16 iliyotokana na tetemeko la ardhi lililotokea Jana Sep 10,2016
 Askofu Kilaini na Sheikh Haruna Kichwabuta pichani
 Sehemu ya Viongozi wa Dini mbalimbali walioweza kushiriki tukio hili la Kihistoria
 Mh. Chiel Kalumuna Meya wa Manispaa Bukoba akitoa Salaam zake za rambirambi kwa wanabukoba
 Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini Mh. Lwakatare akitoa salaam za rambirambi kwa niaba yake na kwa niaba ya Wabunge Wote wa Jimbo la Bukoba na Uongozi wa Chama chake Cha Chadema
 Shukrani kubwa kwao Wafanyakazi wa Chama cha Msalaba mwekundi mkoa Kagera
 Baadhi ya wazee walioweza kushiriki zoezi hili wakibadilishani mawazo
Taswira mbalimbali Uwanjani Kaitaba
 Mkuu wa Mkua wa Kagera akijaribu kupata ufafanuzi kutoka kwa Viongozi wa Dini
 Ndugu Hamim Mahamudu wakati akiwasili eneo la tukio.
Sehemu ya familia za wafiwa katika wakika katika Simanzi kubwa.
 Mwanahabari Faustin Lutta akiwajiba
 Mdau Zack wa Rose Cafe Pichani
 Baadhi ya wadau waliojitokesha kushiriki zoezi hili
 Wadau wakibadilishani mawazo Uwanjani Kaitaba
 Muonekano wa Majeneza yenye Miili ya wapendwa wetu
 Baadhi ya waombolezaji wakiwa Jukwani
 Baadhi ya wafiwa walio ondokewa na Jamaa zao#TetemekoBukoba
Bi Savelina Mwijake Mbunge wa Viti Maalum wakati akitoa Salaam zake za rambirambi
 Baadhi ya Majeruhi wakiendelea kupata matiba katika hospitali ya Mkoa Kagera
 Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa akiendelea kuwafariji Majeruhi waliolazwa katika hospitali ya Mkoa
 Mh.Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwajulia khali wajeruhu waliolazwa hospitalini #TetemekeBukoba
Mh. Waziri Mkuu wakisaliana na Viongozi wa Dini
 Waziri Mkuu akisalimiani na familia za wafiwa

 Muendelezo wa Matukio wakati Mh. Majaliwa akisalimiana na Viongozi wa ngazi mbalimbali
WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ATEMBELEA SHULE YA SEKONDARI IHUNGO KUJIONEA ATHARI ZA TETEMEKO LA ARTHI
Waziri Mkuu Mh.Kassim Majaliwa atembelea Shule ya shule ya sekondari ya Ihungo kujionea athari iliyojitokeza kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea jana tarehe 10/09/2016 katika Mkoa wa Kagera na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Mwanza na Shinyanga.#TetemekoBukoba.
Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa alisema tayari ofisi yake imetuma Wataalamu wa kitengo cha maafa ili kufika Mkoani Kagera kufanya tathimini ya kina na ya haraka wakishirikiana na kamati ya maafa ya mkoa ili kubaini ni sehemu gani zinazohitaji huduma au msaada wa haraka ambapo janga la tetemeko limesababisha madhara makubwa.#TetemekoBukoba
Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa alisema tayari ofisi yake imetuma Wataalamu wa kitengo cha maafa ili kufika Mkoani Kagera kufanya tathimini ya kina na ya haraka wakishirikiana na kamati ya maafa ya mkoa ili kubaini ni sehemu gani zinazohitaji huduma au msaada wa haraka ambapo janga la tetemeko limesababisha madhara makubwa.
 Jengo la Kanisa la Shule ya Sekondari Ihungo likiwa limebomoka kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea jana tarehe 10/09/2016
 Waziri Mkuu Mh.Kassim Majaliwa akiendelea kukagua maeneo ya Shule ya Sekondari Ihungo
 Muonekano wa Ndani wa Kanisa la Shule ya Sekondari ya Ihungo
 Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kuwasiili Mkoani Kagera majira ya saa 7:00 mchana aliwatembelea majeruhi waliojeruhiwa wakati wa tetemeko hilo ambao bado wamelazwa katika Haspitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera, pia alitembelea shule za Sekondari za Nyakato na Ihungo ambako madhara yalitokea makubwa na kupelekea wanafunzi kukosa sehemu za kulala baada ya mabweni yao kubomolewa na tetemeko.
 Vile vile Mhe Majaliwa  alishuhudia maiti 14 na kutoa heshima zake za mwisho kwa marehemu katika uwanja wa Kaitaba ambapo marehemu hao  waliombewa dua na sala kutoka kwa viongozi wa dini Mkoani Kagera . Pia Mhe. Majaliwa aliwapa pole wafiwa na kuzungumza na wananchi waliokusanyika uwanjani hapo kwa kuwapa salaam za Serikali.
  Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Ihungo
Waziri Mkuu Mh.Kassim Majaliwa (katikati) akitoa pole kwa Walimu na Wanafunzi wa Shule ya shule ya sekondari ya Ihungo wakati akipotembelea shule hiyo mapema ya leo Sep 11, kujionea athari iliyojitokeza shuleni hapo
 Waziri Mkuu akisalimiana na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Ihungo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiendelea kukagua athari iliyojitokeza katika shule ya Sekondari ya Ihungo
 Hali ilivyo katika shule ya  Shule ya Sekondari ya Nyakato #TetemekoBukoba
Next Post Previous Post
Bukobawadau