Bukobawadau

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA BUKOBA VIJIJINI ATEMBELEA KATA ZA RUHUNGA NA KYAMURAILE KUFATIA JANGA KUBWA LA NJAA.

 IKIWA ni siku  mbili  baada ya serikali kuanza tathimini ya jinsi ya kusaidia kaya za watu 300 wasiojiweza,wakiwemo Wazee,Wagonjwa,Wajane ,watoto yatima wanaoishi katika mazingira magumu na Walemavu waliokumbwa na tetemeko la ardhi katika mkoa wa Kagera kata ya Kishogo wilaya ya Bukoba vijijini imebainika kuandikisha majina hewa ya nyumba saba kwa lengo la Viongozi wa Serikali za vitongoji na vijiji wajipatie vifaa vya ujenzi kwa njia za udanganyifu.

Udanganyifu huo umebainika katika ziara ya mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Bukoba vijijini Murshid ngeze alipotembelea kata ya kishogo kwa lengo la kuelimisha jamii itambue umhimu wa kubainisha kaya za watu wasiojiweza watakaosaidiwa vifaa vya ujenzi huku akikagua ujenzi wa madarasa mawili ya muda ili kuwapunguzia adha ya kunyeshewa na mvua wanafunzi baada ya majengo kubomoka wakati wa tetemeko la ardhi.
  Mwenyekiti wa halmashauri ya Bukoba Vijijini, Murshid Ngeze akiwahutubia waathirika wa Janga la njaa katika kata ya Kyamuraile.

 Hata hivyo hayo yamebainishwa na diwani wa kata kishogo Deogratias Kaijage na baadhi ya wananchi walisema kuwa orodha ya nyumba zilizoaguka ni nane ila baada ya kuzitembelea amebaini kuwepo kwa taarifa za uongo ambapo Mwandishi wa mtanzania ameshuhudia nyumba moja ya mjane ambaye ameshindwa kuijenga kutokana na umasikini ambae ni Swaumu Isumail maama  mwenye watoto watano na wajukuu watatu kwa sasa wanaishi jikoni.
 Haya ndiyo maji yanatumiwa kwa mahitaji mbalimbali kwa Wananchi wa Bukoba Vijijini
Akitoa elimu kwa wananchi mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya bukoba vijijini  Murshid Ngeze Alisema  kuwa serikali iliyopo madarakani imelenga kumsaidia mnyonge huku mwalimu wa shule ya msingi nyamjunanwa Junias Kashasha aliishukuru kamati ya maafa mkoa wa kagera kwa kujenga majengo ya muda yatakayosaidia wanafunzi kuepuka jua na mvua wakati wa masomo .
“Pasipokudanganyana wananchi wa Kishogo lengo kuu la serikali ya awamu ya tano ni kuwasaidia wahitaji walioathika katika tetemeko la ardhi ndugu zangu tusidanganyane yeyote mwenye uwezo wa kujiongeza katika ujezi kwa pale alipo athilika katika maafa yaliyotukuta ajitahidi ili kupunguza mzigo kwa kamati ya maafa”alisema Ngeze
Theonest Rwetabura mkazi wa kata ya Kishogo alisema kuwa katika zoezi la uhakiki linaloenderea katika jamii yetu ya kuwatafuta wananchi wanaostahili kusaidiwa vifaa vya ujenzi wanatakiwa kuwa wakweli kwa watathimini haina maana kudanganya.
“Niiombe jamii na viongozi wa serilikali za vijiji na kata ili kuwasaidia wenye shida kweli wasio na shida na wamewekwa kwenye utalatibu watajwe hadhalani ili kuondoa dhana ya kuwanyima haki wahitaji wanaostahili” alisema Rwetabura.

Pia alisema kuwa Serikali iwafikilie wale wasiojiweza kwa kaya zenye umasikini uliopitiliza ili kusaidia watu wanaoishi katika mazingila hatalishi maana kuna familia zingine zinakuwa na watoto wenye uwezo na wengine hazingine hazina wasaidizi kabisa.

Mwisho.
Next Post Previous Post
Bukobawadau