Bukobawadau

WAKUU WA MIKOA WAENDELEA KUMUUNGA MKONO MKUU WA MKOA WA KAGERA KUWACHANGIA WAATHIRIKA WA TETEMEKO


     Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhunga

 Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu (Aliyesimama) Akitoa taarifa ya tetemeko kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi aliyekaa


 Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Raphael Muhunga (kushoto)akikabidhi Msaada kutoka Mkoa wa Katavi kwa Mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. Kijuu (Kulia)

  Mkuuwa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu  Akitoa taarifa ya tetemeko kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi aliyekaa


Na Sylvester Raphael

Wakuu wa Mikoa waendelea kumuunga mkono Mkuu wa Mkoa mwenzao katika kuchangia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera ambapo Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhunga amewasilisha michango ya Wananchi wa Mkoa huo jumla ya shilingi 13,909,600/=


Akiwasilisha mchango huo Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Raphael Muhunga alisema kuwa wananchi wa mkoa wa Katavi waliguswa sana na athari za  tetemeko lililotokea mkoani Kagera na wametoa michango yao ili iweze kusaidia katika kurejesha miundombinu iliyoharibiwa na tetemeko hilo.


Mkoa wa Katavi unakuwa mkoa wa pili kuwasilisha msaada kwa waathirika baada ya Mkoa wa Shinyanga ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa wake Mhe. Zinabu Rajab Terack kuwasilisha msaada wa mahitaji mbalimbali wenye thamani ya shilingi 41,172,000/=.


Kipokea msaada huo Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu alimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Katavi pamoja na wananchi wa mkoa huo ambao waliguswa na kuamua kutoa michango yao kwa ajili ya waathirka wa tetemeko katika mkoa wa Kagera .


Aidha Mhe. Kijuu alimweleza Mkuu wa Mkoa wa Katavi kuwa hadi sasa Kamati ya Maafa ya Mkoa wa Kagera kupitia akaunti ya maafa iliyopo CRDB Bukolba  ambayo ni 0152225617300 tayari zimekusanywa shilingi bilioni 4. Pia Mhe. Kijuu aliwaomba wadau mbalimbali ikiwemo mikoa kuendelea kuchangia ili kuurejesha mkoa wa Kagera katika hali yake ya awali.

Mkoa wa Kagera unaendelea kupokea michango kutoka kwa wadau mbalimbali ili kurejesha miundombinu iliyoharibiwa na tetemeko la ardhi lililotokea tarehe 10/09/2016 na kusababisha vifo vya watu 17 na kujeruhi wengine 440, aidha kusababisha nyumba 2,072 kuanguka, Nyumba 14,595 kupata uharibifu hatarishi, na nyumba 9,471kupata  uharibifu mdogo.
Next Post Previous Post
Bukobawadau