Bukobawadau

MKOA WA KAGERA TARATIBU WAANZA KUREJEA KATIKA ENZI ZA NSHOMILE KATIKA ELIMU WASHIKA NAFASI YA TANO KATIKA KUMI BORA KITAIFA DARASA LA VII


Na: Sylvester Raphael
Kutokana na usimamizi na uongozi thabiti chini ya Mkuu wa Mkoa mahili wa Kagera  Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu kiwango cha  Elimu mkoani hapa kimeanza kupanda kwa kasi na kuifanya Kagera kuanza kurejerea katika miaka ya 1980 wakati ule mkoa ulipokuwa unasifikakwa jina la “Nshomile”
Katika matokeo ya darasa la saba ya mwaka 2016 Mkoa wa Kagera umeendelea kufanya vizuri na  kushika nafasi ya tano kati ya mikoa 10 bora, Aidha mwaka 2014 Kagera ilishika nafasi ya 10 kati ya mikoa kumi bora,  mwaka 2015 mkoa ulishika nfasi ya 7 kati ya mikoa 10 bora na mwaka huu umepanda juu nafasi mbili za ufaulu.
Halmashauri iliyoongoza katika mkoa wa Kagera ni Ngara iliyofaulisha kwa asilimia 87.82% na kitaifa imekuwa ya 12, mwaka jana 2015 ilikuwa ya 18. Ya pili ni Biharamulo iliyofaulisha kwa asilimia 85.11% na  kitaifa imeshika nafasi ya 21, mwaka jana ilikuwa ya 3. Halmashauri ya tatu kimkoa ni Muleba liyofaulisha kwa asilimia 83.69% na kitafa kushika nafasi ya 24 ambapo mwaka jana 2015 ilishika nafasi ya 43.
Halmashauri ya nne ni Manispaa ya Bukoba iliyofaulisha kwa asilimia 83.23% na kushika nafasi ya 26 kitaifa aidha, mwaka jana ilishika nfasi ya 47. Ya tano ni Missenyi liyofaulisha kwa asilimia 78.80% na kushika nafasi ya 46, mwaka jana ilikuwa ya 19. Kyerwa ya sita imefaulisha kwa asilimia 77.60% na kushika nafasi ya 53 ambapo mwaka jana 2015 ilishika nafasi ya 68 kitaifa.

Karagwe ya saba iliyofaulisha kwa asilimia 76.79% na kushika nafasi ya 54 kitaifa ambapo mwaka jana 2015 ilishika nafasi ya 72 kitaifa. Halmashauri ya mwisho ni Bukoba iliyofaurisha kwa asilimia 74.86% na kushika nafasi ya 69 kitaifa ambapo mwaka jana ilishika nafasi ya 102, aidha, imepanda nafasi 33 kitaifa japo imekuwa ya mwisho katika mkoa wa Kagera. Shuleiliyoongoza mkoani Kagera na kuwa katika shule 10 bora zilizofanya vizuri kitaifa  ni St. Achileus Chiwanuka kutoka Wilaya Muleba .
Akiongelea matokeo hayo Afisa Elimu Mkoa wa Kagera Bw. Aloyce Kamamba alisema mkoa wa Kagera unaendelea kufanya vizuri na miaka ijayo mkoa huu utaweza kushika nafasi ya kwanza kama ilivyokuwa zamani. Aidha, Afisa Elimu kamamba alisema yeye na wataalam wake watafanya tathmini ya kina kujua kwanini Halmashauri ya Biharamulo imeshuka katika ufaulu ukilinganisha na mwaka jana .
Bw. Kamamba aliipongeza Halmashauri ya Bukoba kuwa pamoja na kushika nafasi ya mwisho katika mkoa kama mwaka jana lakini imepandisha asilimia za ufaulu aidha, imepanda nafasi 33 kitaifa. Bw. Kamamba alisema kuwa juhudi za walimu zimeonekana lakini akatoa wito kwa Halmashauri hiyo kuhakikisha inaongeza juhudi ili iweze kutoka nafasi ya mwisho kimkoa.
Afisa Elimu Mkoa wa Kagera Mwl. Aloyce Kamamba.


Katika hatua nyingine Afisa Elimu Bw. Kamamba alisema mkakati wa mkoa ni kuhakikisha Kagera inashika nafasi ya kwanza kitaifa ambapo yeye pamoja na timu yake ya Elimu chini ya uongozi wa mkuu wa Mkoa wa Kagera wataendelea kufanya usimamizi wa kina ili kuhakikisha kiwango cha elimu kinaendelea kupanda mkoani Kagera.

Mikoa kumi iliyofanya vizuri kitaifa ni Geita iliyofaulisha kwa asilimia 86.92% mwaka jana 2015 ulishika nafasi ya 6. Wa pili ni katavi uliofaulisha kwa asilimia 86.80%, mwaka jana ulikuwa 1, Iringa ulishika nafasi ya 3 na ulifaulisha kwa asilimia 82.87%, mwaka jana ulikuwa wa 10. Dar es Salaam umeshika nafasi ya 4 kwa kufaulisha kwa asilimia 82.59%, mwaka jana ulishika nafasi ya 2. Kagera numeshika nafasi ya 5 kwa kufaulisha kwa asilimia 80.99% na mwaka jana ulishika nafasi ya 7.

Mkoa wa sita ni Mwanza uliofaulisha kwa asilimia 79.13%, mwaka jana ulikuwa wa 3 kitaifa.  Kilimanjaro umeshika nafasi ya 7 na kufaurisha kwa asilimia 79.10%, mwaka jana ulikuwa wa 4. Arusha umekuwa wa 8 kwa kufaurisha kwa asilimia 77.58%, mwaka jana ulishika nafsi ya 5. Njombe umekuwa wa 9 kwa ufaulu wa asilimia 77.10% na mwaka jana ulikwa wa 9. Tabora umekuwa wa 10 kwa ufaulu wa asilimia  71.35% na kushika nafasi ya 10aidha  mwaka jana ulikuwa mkoa wa 25, wa pili kutoka mwisho.
Next Post Previous Post
Bukobawadau