Bukobawadau

WEMA SEPETU AONGEA NA WANAHABARI  ATANGAZA KUAMIA CHADEMA

"Nilipokua kada, nilijitoa muda wangu na maisha yangu. Lakini, nilivyotegemea havikutokea. Sisemi nilitaka kubebwa au la" - Wema Sepetu "Nilizaliwa na kulelewa ndani ya Chama Cha Mapinduzi. Baba yangu alikua kada na alipofariki nadhani aliniachia ukada" - Wema Sepetu .

"Kama nimechukua hata shilingi elfu kumi toka chadema, naomba kaburi la baba yangu lititie kule Zanzibar" -Wema Sepetu "Nimeonewa na nimefanywa nijisikie mnyonge ndani ya chama. Mapenzi ni nipe nikupe, yakiwa ya upande mmoja sio mapenzi"-Wema Sepetu "Nimekuwa nikipewa ushauri & kuonywa kuwa nitafanywa vibaya, nisifanye hivi. Nimeshavaa magwanda sasa, nipo tayari kupigana"-Wema Sepetu  
"Natamka rasmi nimeamua mwenyewe kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenda CHADEMA"- Wema Sepetu "Ni kweli mimi na Wasanii wenzangu tunaidai pesa nyingi CCM. Tukifuatilia tunaambiwa tukamdai Kikwete."- Wema Sepetu

Next Post Previous Post
Bukobawadau