Bukobawadau

MUSHEMBA TRINITY SCHOOL NI TUNDA LINALOCHIPUKIA KAGERA NA TANZANIA

Mushemba Trinity School Bukoba ni shule ambayo ilianzishwa mwaka 2012 ikiwa na watoto 26 hasa wenywe uitaji katika jamii lakini pia kutoka katika familia za kawaida, ni shule ya Bweni na kutwa, ila kwa sasa inapokea watoto wasichana tu kwa ajili ya kulala kuanzia miaka 4 na kuendelea.
 Kwa sasa Shule hii ina watoto 309 na ina darasa la watoto wadogo sana(baby class) Pre.school, darasa la 1-5.Shule hii ni English medium ambayo mkazo wake ni kutumia kingereza na inawalelea watoto katika maadili ya kikristo.
 Shule hii ni mojawapo ya miradi iliyoanzishwa ili kumuenzi Baba Askofu Dr.Samson  Mushemba  pichani kulia ambaye ni Askofu Mkuu Mstaafu wa KKKT NA ASKOFU wa  DKMG
Shule hii ilianzaishwa chini ya shirika la Mushemba Foundation, lenye makao yake makuu Kagera Bukoba, chini ya mwanzilishi wake mkuu  Bwana Josephat Mushemba  ambaye amekuwa akiishi  Denmark lakini akijithidi kuinua swala la elimu kwa watoto wa Kagera.
Madhumuni makuu ya shule ni kuinua kiwango cha elimu kwa  watoto wasiojiweza na wale wanaojiweza ili kuleta uwiano katika jamii bila kubagua mwenye uwezo na asiyena uwezo.
Kwa maana hiyo Mushemba Foundation inafadhili watoto karibia 130 wanaokwenda kwenye shule hii inayoitwa kwa kifupi MTS.
 Wafadhili wa hawa watoto wanatoka  hasa  katika nchi ambayo Josephat anaishi kule Denmark, ambao ni marafiki wake na familia aliyonayo kule dk ni mtandao ambao JOSEPHAT ameujenga kwa miaka mingi akiwa nchini.
Kila mwaka Mushemba ufadhili asilimia 40-50 ya watoto wanaoingia shuleni na asilimia zinazobaki ni watoto ambao wanachngia gharama za masomo.
Shuke hii ambayo kwa mda wa miaka michache Imeonyesha  umahili mkubwa wa kufundisha, walimu wake ni walimu ambao wanapewa training za mala kwa mala , shule ambayo inapokea pia wageni na wafadhili kutoka Denmark ambao uitembelea shule hii mala nyingi kwa mwaka , ambayo uwafanya watoto wapate mda wa kuongea na kuuliza maswali na kujua utamaduni mwingine.
Shule hii pia inajitahidi kufundisha kwa vitendo  licha ya madarasa yao kuwa katika uhodari wa juu sana lakini bado walimu uchukua mda mwingine kuwatoa nje na kuwafundisha kwa vitendo.
Pamoja na hayo shule hii imepata vifaa vyake vyote kutoka Denmark, kuanzia viti meza, black boards kila kitu kimetumwa kutoka nje
 Shule inavifaa mbalimbali vya michezo na shule inasisitiza kwamba watoto wapate mda kiasi wakucheza na vifaa mbali mbali kuburudisha akirim na imeonyesha kuwajengea uwezo mkubw a darasani na kujiamini
Shule pia mwaka jana ilianziasha bustani kubwa inayowalisha watoto mboga za majani  ambazo ni  fresh, hii yote ni kuwajengea watoto lishe nzuri wawapo shuleni  na kuweza kumudu masomo yao shuleni
 Matokeo ya darasa la nne kitaifa yashanganza watu.
Mushemba Triniy school ambayo mwaka  jana  darasa lake kwanza lilifanya mtihani wa kitaifa wa kuingia darasa la Tano, matokeo yake yameshanganza watu wengi, Shule imekuwa ya 3 kiwilaya na 5 kimkoa na Ya 13 kitaifa, kwa matokeo haya shule imeonyesha umahili wake  na kusaidia kupandisha mkoa wetu wa KAGERA KITAIFA PIA, wadau wengi wameipongenza sana shule.
Tarehe 7/2 shule ilifanya  sherehe kubwa siku nzima ambapo walimu walipewa zawadi na watoto wakasherekea ushindi , mkuu Mkurugenzi wa Shule Bwa J osephat Mushemba na mke wake LEA ALIKUWEPO KUWAKABIDHI zawadi walimu na baadae baba askofu mstaafu Dr Mushemba aliongea na watoto na walimu. Ilikuwa ni sherehe iliyoambatana na kwaya za watoto wa shuleni pamoja ngoma .
Shule ina na uwezo wa kubeba wanafunzi wengi  na labda kujaza mpaka darasa la saba kwa sababu  ya facilities zilizopo lakini mkurugenzi wake amekuwa akikisiitiza hatupo kwa ajiri ya kufanya biashara bali kuinua elimu na kuhakikisha tuna fikia viwango.kwa sababu ya watu wengi kuipendelea shule , viongozi wa shule wamekuwa wakiwassitizia wazazi wanaotaka wanafun zi wake kuja Mushemba Foundation  kuomba nafasi mapema sana kuliko kusubiri dakika za mwsiho,
Bibi lena amabaye ni mratibu wa Mushemba Foundation amesema mwaka huu wamerudisha waombi ya watu karibu 70 ambao walikuwa wameomba  nafasi za kujiunga na shule kuanzia january, anasema tumekuwa na wakati mgumu kuwakatalia lakini hatukuwa na jinsi maana kiasi tulivhopanga kila darasa kilikuwa kimetimia
 Director wa Mushemba Foundation Tanzania Mvh hilsen Josephat Mushemba pichani ambaye pia ni muanzili shi Mkuu wa Mushemba Trinity school bukoba akiwapongenza wanafunzi na walimu kwa matokea mazuri ya mtihani wa serikali walipofanya sherehe.
 Walimu na wafanyakazi walioweza kupokea  zawadi kwa ajili ya Ushindi shuleni  hapo.
 Baadhi ya watoto wakiwa darasani katika Majengo ya kisasa kabisa yaliyojengwa hivi karibuni.
 Watoto na wafanyakazi wakisherekea  ushindi kufuatia matokeo mazuri ya shule yao
 Taswira baadhi ya Majengo ya Shule hiyo
 Trinity School rised and became one of the Best Schools In Tanzania according to the latest national exams.
We are so proud of our pupils who worked so hard. Together with the teachers and all other workers at Trinity School we have managed to put Trinity School in a high position in the whole country.
We thank God and give him all the honour for that

 DOWNLOAD Application ya Bukobawadau kwenye simu yako kutoka play store BOFYA HAPA KUDOWNLOAD





Next Post Previous Post
Bukobawadau