Bukobawadau

MBUNGE WA JIMBO LA NKENGE AENDELEA NA ZIARA KIJIJI KWA KIJIJI ....

Mh.Balozi Dr.Diodorus Buberwa Kamala Mbunge wa Jimbo la Nkenge ameendelea na ziara yake ya Kijiji kwa kijiji ambapo leo jumapili July 14,2017 amekutana na wananchi wa Kijiji Kabingo Kata Bugorora ili kutoa mrejesho yaliyojiri katika Bunge la Bajeti sambamba na kusikiliza kero na kutatua changamto zinazowakabili na kutolea ufafanuzi suala la miundombinu ya barabara ya Kyabugombe -Karambi iliyopo chini ya Wakala wa Barabara Vijijini (Tarura) ambapo kiasi cha ambapo kiasi cha Shilingi milioni 924 zimedhibitishwa na Bunge kwa ajili ya Tarura Wilayani Missenyi.
 Wananchi wakazi wa Kijiji cha  Kabingo wakifatilia hoja mbalimbali katika mkutano wa hadhara wa Mbunge Balozi Dk. Kamala
 Wananchi wa Kijiji cha  Kabingo kata Bugorora wakiendelea kumsikiliza kwa makini Mbunge wao Balozi Dk Kamala
 Mh.Mbunge Balozi Dr.Diodorus Buberwa Kamala akitolea ufafanuzi bajeti ya Serikali katika Sekta ya Afya ambapo kuna ongezeko la fedha mara tatu katika mgao wa hospitali za mikoa mbalimbali nchini ikiwemo hospitali kuu ya Mkoa Kagera kutoka Shilingi milioni 700 hadi bilioni 3.1 na kuwaeleza wananchi kwamba Serikali ya Rais Magufuli inazidi kusogeza huduma za Afya karibu na Wananchi
 Mh.Diwani wa Kata ya Bugorora  Projestus Ruzigija akitolea jambo ufafanuzi
 Sehemu ya Wananchi waliohudhuria mkutano huo
Muendelezo wa matukio ya picha
Next Post Previous Post
Bukobawadau