Bukobawadau

KAMPUNI YA UBELGIJI YA TPF SAMBRE YAANZA KUFANYA KAZI TANZANIA

Balozi wa Tanzania Ubelgiji Dr. Diodorus Buberwa Kamala (wa pili kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa kampuni ya ushauri ya TPF Basse Sambre baada kukutana nao leo ofisini kwake Brussels. Wa kwanza kulia ni Bwana. Stefan Pousset Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo na wa kwanza kushoto ni Bwana Jerome Bestgen Meneja wa mauzo wa kampuni hiyo. Wa pili kulia ni Bwana Nyamtara Mukome afisa katika Ubalozi wa Tanzania Ubelgiji. Wawakilshi hao walimweleza Balozi Kamala  kwamba wamepata shughuli za kufanya Tanzania na wanatarajia kufungua ofisi zao Tanzania. Balozi Kamala aliwashauri watafute Watanzania wa kushirikiana nao  ili kampuni yao iweze kuimarika, kuhimili ushindani katika sekta ya ushauri, kutoa ajira na kusaidia kujenga uchumi wa Tanzania.
Next Post Previous Post
Bukobawadau