Bukobawadau

CLUB MPYA KUFUNGULIWA KWA MAMA ANNA TIBAIJUKA

Hivi ndivyo linavyo onekana Jengo la hotel mpya na club mjini Mleba.Ni 'Waisuka' night club, iliopo kwenye jimbo la Mama Anna Tibaijuka;ambaye ni Waziri wa nyumba na makadhi.Club hiyo ipo katika hatua za mwisho za ujenzi.Na inatalajiwa kufunguliwa rasimi tarehe 4.6.2011 kwa mujibu wa muhusika Ndg.Mitti mwenyeji wa mleba na mwenye makazi yake mjini kigoma.

Mwonekano wa sehemu za ndani upande wa club ndio kama hivi katika picha, kazi kwenu wapenda burudani,shangwe na mikasarukasa kiwanja ndo hicho hapo.

picha inaonyesha sehemu za ukumbini,kama unavyojionea hiyo stagi.

Kila ukizunguka ubavuni mwa jengo unakutana na garden,au waweza kuita floriculture na kwa kiswahili fasaha tunasema bustani.

Hii ni sehemu inayo endelea kutengenezwa kwa ajiri ya maegesho ya magari na vyombo mbali mbali vya usafiri.Picha na matukio yote by mc.
Next Post Previous Post
Bukobawadau