Bukobawadau

HII NI NYAMKAZI-MIKOCHENI YA BUKOBA ;Unaweza usipapende kwa msimu huu wa Senene kwani Mazingira na Changanyikeni uzua taflani.....!!!!!!

Hivi sasa wale wadudu maarufu jamii ya panzi yahani senene ni wa kumwaga hapa mjini bukoba,

Pia Mgao wa Umeme tunausikia kwenye vyombo vya Habari sisi tunatumia umeme kutoka nchini Uganda

Hapa mbali na matatizo ya ukosefu wa fedha kama wabongo wengine lakini kwa hayo tunakula maisha

Pichani ni namna senene wa taa wanavyo windwa.
Kwa kuwa senene upendelea kusogea karibu na mwanga mkali hivyo wenyeji wa maeneo haya uandaa mazingira ya kuweza kuwakamata kilahisi ,senene akijigonga kwenye bati useleleka kwenye pipa na ni vigumu kujinasua kwani wanamiminika kwa wingi na kwa kasi kubwa.

Hii ni barabara inayo elekea shule ya sekondari ya Nyanshenye.
Hali ya mazingira inaonekana hivi wadau wametega senene.

Mapipa na Mabati yamewekwa katika hali ya utayali kutumika jioni ya leo kwa kutega au kukinga senene.
Majaba ya senene walio chemshwa.
Usiku hali inakuwa hivi
Next Post Previous Post
Bukobawadau