Bukobawadau

WADAU HEBU ANGALIA HALI YA MAISHA ILIVYO NGUMU!!!!!!!!!NA NIKAWAIDA KWA MAENEO YA RUBALE,ICHWANDIMI NA NYAKIGANDO

Hii ni maiti ikisafirishwa kutoka Ndolage hosp.kuelekea kijijini Ichwandimi hali hii inaweza kukushangaza ila hii ni hali ya kawaida kwa wakazi wa Rubale na Nyakigando,na Misenye.
Hii ni baada ya kumfata kwa nyuma na kumsimamisha baada ya kua ametupita kwa mwendo usio wa pole pole.
Baada ya Kuongea nae na kutueleza kuwa yeye amekodiwa na jamaa mmoja alie fiwa na mke wake hii ni maiti ya Mwanamke. Ndg Mdau bukobawadau tumeguswa sana na hali hii tena katika maeneo ambayo si vijijini sana unapo ongelea Ndolage ndio kamachumu,Bukoba,Ibwera,Nshamba na Muleba ...wadau ni nini mtazamo wenu juu ya hili.
Kwa wale wanao yajua maeneo haya jamaa alitupita kwa mwendo kasi tukiwa Ibula tukaja kumpata akiwa mwanzoni mwa kijiji cha Rutenge.
Tukiwa tunazidi kumfukuzia...kwa karibu.
Next Post Previous Post
Bukobawadau