Bukobawadau

MEYA WA MANISPAA MH. ANATORY AMAN AFUNGUA RASMI SEMINA YA MAFUNZO YA UJASILIAMALI

Meya wa Manispaa ya Bukoba Mh. Anatory Amani kulia akifatilia mafunzo  yanayotolewa kwa wadau wajasiliamali walio hudhulia hii leo kwenye ukumbi wa St.Francis  uliopo Miembeni Bukoba.
Mh Chief Diwani wa Kata ya Kahororo na Ndg Meda Mkurugenzi wa Victorious Hotel nao ni sehemu ya wadau walio hudhulia semina hii.
Swala zima likiendelea kwa nadharia na vitendo
Kwa usikivu mkubwa wanaonekana wadau wakisikiliza hatua muhimu za utengenezaji wa sabuni za maji, shampoo na mishumaa.
Mkufunzi akiendelea kutoa somo.
Mafunzo haya  yamehusisha wajasiliamali wa jinsia zote na rika zote.
 Namna mjasiliamali  Kipofu wa macho anavyo mudu kuandika maelekezo anayo yapata,.
Mdau Ndg Kamu maarufu kwa jina la Diamond.
 Mwonekano wa wadau mbele ya meza kuu.
Hapa anaonekana Mdau Mc Baraka katika pitapita  ili kupata kitu kamili cha kukufikishia bila zengwe!!!
 Semina hii itaendelea tena kwa siku mbili muda ni kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 8:00 Mchana na 8:00mchana hadi saa12:00 jioni.

Form za ushiriki zinapatikana;
-Kamachumu Shop mkabala na Duka la Nyegera Waitu
-New PK Studio mkabala na Kagera Studio.
 Stend kuu ya Mabasi ndani ya Duka la Kilibata.
-Soko Kuu kwa Nje -Masikini halali Mchana.


Next Post Previous Post
Bukobawadau