Bukobawadau

HALI YA VURUGU ZANZIBAR IKIWA IMEANZA KUA SHWARI WADAU MBALI MBALI WATOA MAONI YAO KUFATIA KITENDO VYA KUCHOMA MOTO KANISAA

Hali ikiwa shwari hii leo.
Maelfu wa Wazanzibari wakiongozwa na Taasisi za Kiislamu na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar JUMIKI, wakifanya matembezi ya amani katika barabara za Zanzibar na kupeleka ujumbe wao kwa viongozi wa Serikali ya Zanzibar na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Umoja wa Mataifa wakitaka Zanzibar huru, ambapo baadhi ya watembeaji hao wakiongozwa na Kiongozi wa Jumuiya hiyo, Sheikh FARID HADI AHMED na viongozi wengine.




MAONI YA WADAU MBALIMBALI
  • Christopher Kaijage kuna nini katika muungano huu .??kama ni suala la usalama sisi tunayo majeshi ya kulinda usalama sio mpaka zanzibar iwe ndani yetu hata hivyo bado tunawaonea zanzibar tuwaache wajitawale kwani kwa sasa wanawasomi wa kutosha wanazo maligafi za kujitunza na pia sijui kama itakuwa safi kama wakitumuliwa hapa kariakoo maake ndo inawabeba , nawashauri ndugu zangu viongozi wapeni uwezo zanzibar wajitawale kabla suala la udini alijaanza "jihad"inanukia sasa

  • Prudens Rweyongeza Sasa Makanisa yanahusika vipi na kero za Muungano??? Watu wanatumia fursa hizi za machafuko kutekeleza mambo yao ya chuki dhidi ya wenzao! Hizi dhambi zitawatafuna hata kama ikitokea wakajitenga, kamwe hawataishi kwa amani!
     
      
     Statement  ya Zitto Kabwe

1 .Vurugu za Zanzibar ni 'unwanted distractions' katika mchakato wa kuandika katiba mpya.

2. Hakuna namna vitendo hivyo vinaweza kuhalalishwa na kutetewa lakini ni matokeo ya muda mrefu ya 'superficial attempts at dealing against groups with ulterior motives.

3. Rais Ali MohamedShein aunde kikosi kazi maalum kwa ajili ya kudhibiti vurugu hizo,na kuanza mzungumzo na pande zote.Hiki sio kitendo cha kudharau kabisa

4. Muungano wetu ni sacred na tumetoka mbali kushindwa sasa kuulinda, 'not when we are so close at having an everlasting formula'

5. Waliochoma nyumba za ibada wasakwe na kufikishwa mbele ya sheria mara moja. Tusiruhusu hata kidogo wapuuzi wachache kutuingiza katika vurugu za kidini ili kufikia malengo yao ya kisiasa.

6. Zanzibar Political leaders and public opinion makers must engage the Zanzibaris into a serious and objective dialogue about the future of Zanzibar within or outside the Union.
Next Post Previous Post
Bukobawadau