Bukobawadau

MASHABIKI WA CHELSEA MJINI BUKOBA WASHEREKEA KUTWAA UBINGWA WA LIGI YA MABINGWA ULAYA KWA KUTOA MSAADA KWA WATOTO YATIMA NA BADAE KUENDELEA NA SHEREHE KATIKA UKUMBI WA LINAS NIGHT CLUB

Anaonekata Mwenyekiti wa Mashabiki wa Chelsea wa Mjini hapa akitoa shukrani kwa Mlezi wa Kituo cha Watoto yatima.
 Wanaonekana Mashabiki wa Chelsea wakiwa wamebebelea kile walichokiandaa tayari kwa kukabidhi kwa mhusika wa Kituo hiki kilichopo Kashai  msaada huo ni  Chakula, Mafuta ,Sabuni, Biskuti na Pipi.
 Walitumia fulsa hii  kutembelea baadhi ya maeneo ya kituo hiki na kubadilishana mawazo na Watoto hawa pichana anaonekana Mdau Faraji akichukua matukio ili kuweka kumbukumbu.
 Shangwe zikiendelea kituoni hapo, Mavuvuzela yakisikika.....!!!
Hakika uhungwana ni Matendo.
Wameshiriki michezo mbali mbali na Watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha Kashai.
 Mafans wa Chelsea katika picha ya pamoja na Watoto Yatima na  Mlezi  wa Kituo na baada ya hapo wakaendeleza furaha yao kwa kuzunguka mitaa kadhaa ya Mji wa Bukoba kwa maandamano na msafala wa Magari na Pikipiki.


BUKOBAWADAU BLOG TUNATOA PONGEZI KWENU  KWA  KUWAKUMBUKA WATOTO YATIMA !!!!

Msafala wa Mafans wa Chelsea ikiwa ni mtaa kwa mtaa  hii barabara ya Jamhuri.
Mdau Imani kwa raha zote.
 Bonge la sound watu na raha zao
 Vitimbwi katikati ya Mji
Yote juu ya yote mashabiki hawa wa Chelsea  wakiongea na Bukobawadau katika EXCLUSIVE INTERVIEW wameonyesha kusononeka  "Drogba kuiacha timu yao"!!!
Kidedea kimechaniza pande za Buyekela, Nyakanyasi,Hamugembe, Rwamishenye,Mjini kati barabara za Kashozi, Jamhuri na tupendane na pande za Kashai,

NI MWENDELEZO WA HABARI MATUKIO NAMNA MASHABIKI WA CHELSEA WALIVYOSHEREKEA KUTWAA UBINGWA WA LIGI WA MABINGWA ULAYA.!!!!!!!!
Wadau katika kutambulishana .
Ndani ya Ukumbi wa Linas Night Club Sherehe iliendelea, kwanza walifanya utambulisho kwa walio hudhulia
ikiwa ni pamoja na wageni waalikwa,Mdau pichani ni Mwanainda Hamza.
 Anaitwa Edwini I shengoma.
 Ni fans Issack Isaka.
 Mdau akifanya Utambulisho
Anaitwa Mbaraka Omary ni mtangazaji 88.5 Kasibante FM Radio. Ni fans babu kubwa wa Chelsea, kazi yake anaijua, anaweza na yote juu ya yote anaipenda,Mbaraka ni muamasishaji mkubwa wa shughuli hii.
Shaban Kaluani sehemu ya waalikwa.
 Anaitwa Bi Salome aka Chui na London, mambo yake siku zote ni tofauti kabisa hapa anatiririka mayai mm!
 Mwenyetabasamu pana na Simu mkononi ni Bi Rukia na mwenye mwili mpana na mng'avu usoni ni Kaka Mkuu ,wao ni waalikwa katika shughuli hii
 Katika Intro. Mdau Edgar Konyani.
Kwa uzuri wa tukio na ukali wa picha najikuta nashawishika kuendelea......!!!!!
 Ni Vijana wa Kajuna kulia ni Mdau Hamary.
Iko pooawa JEMBE.!!

BAADA YA ZOEZI ZIMA LA UTAMBULISHO KUKAMILIKA , SHEREHE IKAFUNGULIWA RASMI NA MWENYEKITI WA CHELSEA BUKOBA BI MAINDA KASSIM
Mwenyekiti akitekeleza kwa kueleza kile kilichokusudiwa hapa nimependa MC mwenzangu jina kapuni alivyoweka tega!!!!
Mwonekano wa Keki husika.
Ni watoto wa Mzee Shabani Zakalia wa Katatolwansi wakishiriki kikamilifu kukata keki.
Champagne kadhaa zilifunguliwa Over tupo Stamford Bridge !!!
Wakigonga Cheers kwa furaha.
Mdau Mtensa Leonard 
Ni wasaa wa kupata Msosi ,pichani  wanaonekana Wageni waalikwa wakipata huduma,Kaka Malick Batalingaya  nae ndani.
Mdau Rukia na Bi Salome
Huduma ya Chakula ikiendelea
Miembeni Moja Ilikua!, na  Tanga tumezaliwa!!!!!!!!
BAADA YA CHAKULA NI BURUDANI JAPO SITOKEI TANGA!!!!
Bhampa 2 Bhampa kama kawaida !!!!
Mafans kataika picha ya Pamoja..
MWISHO NIKUOMBE MDAU MSOMAJI KUPITIA MATUKIO YA MUDA MCHACHE ULIOPITA KWA KUGONGA NENO OLDER POST KILA  MWISHO WA PAGE.



Next Post Previous Post
Bukobawadau