KAMATI YA BUNGE YA SHERIA NDOGO YAWASILI KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE MKOANI KAGERA
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Sheria Ndogo Wakiongozwa na Mwenyekiti Wao Mhe. Sylvester Mabumba Wakiwa Katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mh. Fabian Massawe
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Akiwapa Maelezo ya Utangulizi na Halisi ya Mkoa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Sheria Ndogo
Kamati ya Bunge ya Sheria Ndogo inayoongozwa na Mwenyekiti wake Sylvester Mabumba pamoja na wajumbe wake wapo mkoani hapa kupitia, kuona na kuchambua sheria ndogo katika Halmashauri za Wilaya za mkoa wa Kagera ili sheria hizo kupitishwa kwa ajili ya kutekelezwa.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Akiwapa Maelezo ya Utangulizi na Halisi ya Mkoa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Sheria Ndogo
Kamati ya Bunge ya Sheria Ndogo inayoongozwa na Mwenyekiti wake Sylvester Mabumba pamoja na wajumbe wake wapo mkoani hapa kupitia, kuona na kuchambua sheria ndogo katika Halmashauri za Wilaya za mkoa wa Kagera ili sheria hizo kupitishwa kwa ajili ya kutekelezwa.
Aidha
kamati hiyo ipo hapa mkoani kuona changamoto zilizopo katika kutekeleza sheria
ndogo za Halmashauri za Wilaya au ni wapi sheria hizo zinakwamishwa, na kotopitishwa
kwa wakati ili ziweze kutekelezwa kwa wakati .
Akitoa
ufafanuzi wa kutekeleza sheria ndogo katika mkoa wa Kagera Mkuu wa Mkoa mbele
ya Kamati hiyo katika ofisi yake, alisema pamoja na upungufu wa watumishi
katika Halmashauri za Wilaya lakini sheria ndogo mkoa wa Kagera zimeweza
kurekebishwa na kuenenda na mazingira ya kukusanya mapato.
Pia
mkoa wa Kagera umeweza kutunga sheria ndogo ya kuunda mfuko wa elimu na baadhi
ya Halmashauri za Wilaya tayari zimeunda mifuko hiyo. Sheria ndogo ya
kuhakikisha wananchi wanatekeleza usafi katika maeneo yao, aidha sheria hizo
zinaibuliwa kutoka kwa wananchi wenyewe na wananchi wana mwamko wa kuitikia
kutunga sheria hizo ndogo.
Pamoja
na mafanikio hayo lakini Mkuu wa Mkoa alibainisha pia changamoto katika kutunga
sheria ndogo, kuwa ni upungufu wa Wanasheria katika Halmashauri za Wilaya,
sheria ndogo kuchelewa kuidhinishwa ili zitekelezwe kwa wakati, baadhi ya
sheria ndogo kupitwa na wakati, pia baadhi ya sheria ndogo kuwabana wananchi
hivyo kutokea sheria hizo kuchukiwa na jamii.