Bukobawadau

WATU WATATU WAKAMATWA NA BUNDUKI NA RISASI 96 SERENGETI

na pascal michael buyaga
serengeti

Watu watatu wakazi wa kijiji cha motukeri katika wilaya ya Serengeti mkoani mara,akiwemo raia wa nchi ya Kenya wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani mara kwa tuhuma za kukamatwa na bunduki aina ya smg Fn na risasi 96 kinyume cha sheria.
Kamanda wa polisi wa mkoa huo kamishina msaidizi  Absalom mwakyoma amethibitisha kukamatwa kwa watu hao ambao amewataja  kuwa ni  sabasaba makuru kambarage (31),Timothy Bernad omoke (20) raia wa Kenya na pius mayengo sengeka( 43) wote wakiwa wakazi wa kijiji hicho kilicho kata ya nata wilayani Serengeti.
Kamanda mwakyoma amesema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa octoba 23  majira ya saa mbili na nusu usiku mwaka huu katika kitongoji cha mageriga nyumbani kwa mtuhumiwa wa kwanza sabasaba wakimiliki silaha hiyo ya kivita  kinyume cha sheria
Amesema kuwa Maafisa wa polisi wakishirikiana na maafisa wa shirika la hifadhi Taifa (TANAPA)siku ya tukio baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema walifanya msako na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa na vipande 10 vya nyama kavu  ya  pori ,mikia sita ya nyumbu na mayai mawili na maganda mawili ya mayai ya mbuni kinyume cha sheria ambapo thamani ya nyara hizo hajafahamika.
“ Polisi wakiwa katika msako mkali wa kuwasaka wahutumiwa hao walifika kijijini hapo majira ya saa mbili na nusu usiku ndipo waliwakuta ndani ya nyumba hiyo walimokuwa wakihifadhi nyara hizo na kisha kufanikiwa kuwakamata”alisema kamanda mwakyoma.
Inadaiwa kuwa bunduni hiyo imekuwa ikitumika kuulia wanyama pori na wakati mweingine vitendo vya uharifu sehemu mbalimbali hapa nchini na kuhatarisha usalama  na maisha ya wananchi pamoja na mali zao.
Kamanda alisema kuwa  upelelezi utakapo kamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria na ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi  kufichua na kuwataja  waharifu.
Next Post Previous Post
Bukobawadau