Bukobawadau

MATAPELI SUGU WAAMBULIA KICHAPO BAADA YA DEAL KUSANUKA!!

 Watu wawili  Mwanaume na mwanamke wanaotuhumiwa kwa Utapeli wameambulia kichapo kikali  kutoka kwa wananchi wenye hasira baada ya kugundulika  wanataka kumtapeli Mama mmoja kwa kutumia mbinu ya kumuonyesha DHAHABU FEKI kwa madai kwamba wao ni wageni mjini na wanahitaji msaada wa pesa wao wakupe hiyo dhahabu ikiwa imefungashwa kwenye kifuniko angavu na kitambulisho cha udhibitisho,kama utakavyo ona pichani.
Wakati bado matapeli hao wanaeneleza mchakato wa kumpa somo huyo mama,akatokea msamalia mwema aakasaidia kumuelewesha kwa lugha nzuri kuwa jamaa wanataka kumuibia.


Askari Polisi wenye dhamana ya kulinda Usalama wa Raia na Mali zao wanafika eneo la tukio.
 Anaonekana mmoja wa Polisi wa Usalama barabarani akiingilia kati kuwazuia Raia wasiendeleze kichapo.
Moja ya mbinu wanayo itumia ni pamoja na kuonyesha kitambulisho hiki  pichani chenye maneno ya kutamanisha wakati lengo lao ni kurekebisha tamaa yako!!
Hiyo ndiyo sample wanayotumia  kama dhahabu
Umati mkubwa wa mashuhuda wa tukio hili
Ingia uko..Mmxxxxx!!
Hii ndiyo hali halisi Mdau hapo zamani walisema mjini shule ila kwa sasa unaambiwa MJINI MIPANGO kupitia tukio hili unaweza KUFUNGUKA na kujua mbinu wanazotumia matapeli mtaani ingawa staili hii ya dhahabu wengi wanaijua kwa kuwa imetumika kwa muda mrefu, angalizo letu Bukobawadau  ni kwamba zipo nyingine nyingi unaweza shawishika hivyo tuwe makini
Next Post Previous Post
Bukobawadau