Bukobawadau

ABIRIA WA NDEGE MJINI BUKOBA WAKWEA BUS KUFUATIA RATIBA KUTOKUELEWEKA

 Habari zisizo RASMI  zinasema kutokueleweka kwa ratiba za NDEGE  mjini hapa ni kutokana na ukarabati na upanuzi  wa uwanja huu wa ndege kwa kiwango cha lami, hivyo uwenda  ukafungwa kutumika kwa muda.
 Camera yetu ikiangaza kipande chenye lami, uku mvua ikiendelea kunyesha na kufanya wahusika wapate sababu ya hali ya hewa ingawa tatizo la ratiba limejirudia  kwa siku ya pili pasipo mvua kunyesha wala wingu kutanda!!
Baadhi ya abiria wanaoelekea jijini Mwanza kwa ndege ya shirika la ndege la Precision Air wakiwa katika sintofahamu  baada ya kushindwa kusafiri kwa siku ya jana kwa mujibu wa ratiba ilivyokua na pasipo kupewa ujumbe wowote kama inavyoeleweka ,kwa dhana wangesafiri badae ama siku inayofuata.
 Uku wakiwa wamepoteza mwelekeo na kuwaladhimu wengine kukodi magari binafsi na wengine kukwea bus lililofika uwanjani hapo.
 Mdau Ibra  ambaye ndiye dereva wa bus la Minziro kwetu linaloelekea Mwanza kwa kila siku akiwa katika utayari wa kuanzisha safari.
Muonekano wa kipande cha lami katika Uwanja wa Ndege wa Manispaa ya Bukoba.
Next Post Previous Post
Bukobawadau