Bukobawadau

KATIKA KUWATIA WAISLAM WOTE IJUMAA NJEMA-SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA YA ZANZIBAR YAPIGA MARUFUKU CD ZA ROGO,UAMSHO NA ILUNGA.

Muonekano wa Msikiti wa Ijumaa Mjini Bukoba
Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar inayoongozwa na Dr Shein na Makamo wake Maalim Seif kupitia Jeshi la Polisi wamepiga marufuku rasmi cd zote za mawaidha ya Kiislam za UAMSHO,MUJAHID ABOUD ROGO na SHEIKH ILUNGA.

Hayo alisema ocd wazamani Murtad MKADAM ambae kwasasa yupo ofisi kuu ya polisi kitengo cha madawa ya kulevya Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif.

Alisema cd hizo za kiislam ni chanzo cha uvunifu wa amani hapa nchini na ndio zinazosababisha uchochezi baina ya dini ya ukiristo na uislam. Akifafanua alibainisha kuwa mpaka sasa washawakamata watu kadhaa wanaojihusisha kuuza cd hizo na kuwaonya wale wote ambao huweka kuzisikiliza watachukuliwa hatu kwani serikali ina mkono mrefu.

Akijibu baadhi ya maswali aliyoulizwa kwamba waliowakamata hawawaoni kuwa wamewadhulumu kwa kufanya biashara halali ya uzaji cd. alijibu cd zile za mawaidha ni Haram wala sio rizki ya halali kwa upande wa serekali kwani zinapelekea uvunjifu wa Amani katika nchi.
Next Post Previous Post
Bukobawadau