Bukobawadau

PICHA NA MATUKIO MBALIMBALI

BABA John wa Bk na Mwana wa Kaiza ,wakicheck na Camera yetu ughaibuni
 Hivi ndivyo Msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Fleva, Joseph Haule, (Prof. Jay) alivyo jiunga rasmi leo na chama cha CHADEMA.
 NYEPESI NYEPESI TULIZONAZO JUU YA UJIO WA JIGGAR
Bado wataalam wa mambo wanaendelea kutofautiana kuhusu ratiba ya Tour ya Jay – z iliyotolewa na Billboard hivi karibuni katika ratiba hiyo imeandikwa Jay z atatua katika miji 7 ya Africa ikiwemo jiji la Dar es salaam Oktoba 4 mwaka huu pale Diamond Jubilee. Ratiba hiyo inatia shaka kwa sababu Jay z aliperform tarehe na mwezi kama huo Dar es salaam mwaka 2006 na katika website ya Jay za ametoa ratiba ya Tour zake lakini ameishia kuandika mwezi Septemba, hajaandika mpaka Oktoba kama walivyoandika Billboard


 Tanzania imepata hasara ya dola bilioni 1.8 za kimarekani kwa mwaka jana kutokana na ukosefu wa ufanisi bora katika bandari ya Dar es Salaam, ambapo kwa mujibu wa ripoti ya benki ya dunia kama hatua za kuboresha ufanisi katika bandari hiyo zitachukuliwa na rushwa ikapungua ,uchumi wa tanzania utainuka kwa kiasi kikubwa.
Rais wa Marekani Bw. Baraka Obama na Mkewe wanatarajia kufanya ziara ya nchi tatu barani Afrika itakayojumuisha nchi za Senegal, Afrika ya Kusini na Tanzania, Kuanzia tarehe 26 Juni hadi tarehe 3 Julai. 

Katika ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, uwekezaji na biashara, uimarishaji wa taasisi za kidemokrasia na uwekezaji katika kizazi kipya cha viongozi wa Kiafrika.

Rais atakutana na viongozi mbalimbali wa kiserikali, sekta binafsi na jumuiya huru ya kiraia ikiwemo vijana ili kujadili ubia wetu wa kimkakati katika ushirikano wetu rasmi na masuala mengine ya kimataifa.
 
Ziara hii itadhihirisha dhamira ya dhati ya Rais ya kupanua na kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na watu wa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika kuimarisha amani na ustawi katika kanda hii na duniani kote kwa ujumla

 MJINI BUKOBA Wajanja wote wanasikiliza Vision fm radio 100.OMHz kutoka KIBETA, BUKOBA-TANZANIA karibu utusikilize katika msimu huu mpya wa mapinduzi ya utangazaji na masuala mazima yanayohusu burudani hapa Kagera na tuunge mkono kwenye kampeni ya kuinua uchumi na maendeleo ya wana Kagera na hasa Vijana ambao ndio taifa la leo ambalo mara zote wamekuwa na changamoto nyingi za kuanza maisha na kuyafanya kuwa "BORA"

VISION FM RADIO 100.0MHz "ONGEZA MTAZAMO"

 Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anna Kilango akizozana na mnadhumu wa kambi ya upinzani, Tundu Lissu nje ya ukumbi wa Bunge baada ya Spika kuahirisha Bunge akiagiza hotuba ya kambi ya upinzani kuhusu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kufanyiwa marekebisho.Picha na Emmanuel Herman
Next Post Previous Post
Bukobawadau