Bukobawadau

PICHA ZILIZOTUFIKIA NA HABARI MBALIMBALI KWA MKUTASARI

Viongozi wetu wakifurahia jambo hii ni picha iliyotufikia.
Ustaadh huyu pichani , akiwa katika mizunguko yake wa kutafta futari, ni maeneo ya stend kuu ya mabasi Mjini Bukoba,cha kufurahishwa waungwana wameweza kumtimizia
#‎KAGASHEKI‬ CUP 2013  NDANI YA UWANJA WA KAITABA
Mchana wa leo tImu ya Bakoba yaendeleza ubabe kwa kuwasimamisha kahororo kwa mabao 3-0
‪#‎Mchezo‬ wa pili jioni hii HAMUGEMBE 3-1 NYANGA


 Taswira katika picha mbalimbali za shughuli ya mapokezi
Miili ya wanajeshi saba mashujaa wa Tanzania waliofariki wakiwa kazini wakitekeleza ulinzi wa amani wa kimataifa katika mkoa wa Darfur nchini Sudan, imewasili leo kwa ndege maalumu ya Umoja wa Mataifa.

Kaimu Mkurugenzi wa habari wa JWTZ, Meja Joseph Masanja amesema miili hiyo imewasili leo Jumamosi majira ya saa 9.45 alasiri katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa JNIA na imehifadhiwa katika hospitali ya jeshi ya Lugalo hadi Julai 22 ambapo itaagwa rasmi.

Miili iliyowasili ni ya Sajenti Shaibu Othuman, Koplo Oswald Chaula, Koplo Mohamed Juma, Koplo Mohamed Chikilizo, Pte. Rodney Ndunguru, Pte. Peter Werema na Pte. Fortunatus Msofe.

Shughuli za kuagwa miili ya wanajeshi hao zitafanyika katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga taifa vilivyoko Upanga jijini Dar es salaam.

Kuwapoteza wanajeshi hawa ni la kwanza na kubwa kwa nchi ya Tanzania tangu Tanzania ilipoanza kuchangia walinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa mwaka 2007. Wanajeshi wengine watatu wa Tanzania walifariki dunia mwezi uliopita baada ya chombo chao cha kusafiria kusombwa na maji ya mto uliokuwa umefurika huko nchini Sudan. 


Miili ya askari saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)wakio uawa huko Darful yawasili
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti cha utambulisho wa Ukufunzi wa Kozi maalum ya Kwanza ya Mafunzo, katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) Dkt. Regnald Abraham Mengi, wakati wa sherehe za kufunga Kozi hiyo zilizofanyika katika Chuo hicho, Kunduchi jijini Dar es Salaam, leo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti cha kuhitimu Kozi maalum ya Kwanza ya Mafunzo, katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) ACP Charles Omari Mkumbo, wakati wa sherehe za kufunga Kozi hiyo zilizofanyika katika Chuo hicho, Kunduchi jijini Dar es Salaam, leo.
Mhe. Mwigulu Nchemba akiwa na familia yake
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti cha kuhitimu Kozi maalum ya Kwanza ya Mafunzo, katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) Hassan Khatib Hassan, wakati wa sherehe za kufunga Kozi hiyo zilizofanyika katika Chuo hicho, Kunduchi jijini Dar es Salaam, leo.
Rais Uhuru Kenyatta akifuturisha Ikulu ya Nairobi

MISELE YA HAPA NA PALE,NI SHUGHULI YA KIJANA MANSURY NDANI YA STEND YA MABASI MJINI BUKOBA
‪#‎ekigale‬
Next Post Previous Post
Bukobawadau