Bukobawadau

TASWIRA MJINI BUKOBA MAENEO YA SENETI YALIVYO POKELEWA MAAMUZI YA NAPE !!.

Katikati ya viunga vya bukoba,nje ya soko kuu kijiwe mama cha seneti kinacho ongoza kwa mitazamo ya kisiasa ya chama tawala hivi ndivyo wadau walivyo guswa na maamuzi ya Nape ya kwamba'Kwa mujibu wa utaratibu wa kutoa adhabu kwa viongozi wa CCM walio kwenye vyombo vya dola hasa Wabunge na Madiwani uamuzi wa Halmashauri Kuu ya Mkoa sio wa mwisho. Uamuzi huo unapaswa kupata Baraka za Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ndipo utekelezwe'.
 Bi Jeanifer Murungi Kichwabuta  mmoja wa madiwani katika sakata hili,(viti maalum ccm)
 akifurahia maamuzi ya Nape  kulia ni mwanahabari  Audax Mtiganzi
Wadau wakicheck na Camera yetu nje ya soko kuu mjini Bukoba.
Ni kufuatia maamuzi ya Nape kwamba mpaka sasa Madiwani hao wanane waliosimamishwa wanapaswa kuendelea na kazi zao kama kawaida wakisubiri kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kitakachoketi tarehe 23 Agosti, 2013 mjini Dodoma ambacho pamoja na mambo mengine kitapitia uamuzi huo wa Halmashauri Kuu ya Mkoa wa Kagera.
Mdau Bushira mwenye joho la kinegeria akibadilishana mawazo na Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa Ndg Abdul Kagasheki (Kananga)


Diwani Jeanifer na Diwani Bigambo.
Mh. Bigambo akiendelea kutolea jambo ufafanuzi
Ndugu Ramadhani Kambuga Katibu mwenezi wa CCM Bukoba mjini


 Pichani anaonekana Diwani wa kata ya Bakoba Felician Bigambo (CUF) akiongea na wananchi juu ya kile kinachoendelea katika sakata hili na namna alivyoyapokea maamuzi ya Nape.
Anaonekana Ndg Mshamu aliyekaa akiwajibika wakati huo wadau wengine wakimsikilizaa Bigger One Mh Bigambo
Diwani wa kata ya Kashai ambaye pia ni mwenyekiti wa wilaya Bukoba mjini akipongezwa na wananchi muda mfupi baada ya maamuzi ya alimashauri kuu ya ya mkoa kutenguliwa hapo jana
Picha na Faustini Rutta.
Next Post Previous Post
Bukobawadau