Bukobawadau

HAPA NA PALE NA CAMERA YETU LEO IJUMAA SEPTEMBA 13, 2013 RUBYA, BUGANGUZI ,MULEBA

 ASUBUHI NJEMA KWAKO MDAU KUTOKA RUBYA MULEBA 'MIANDA ATANO'...maarufu kama Sanamu ya Mfano wa Bikila Maria 'Kyanya'
Mdau akichukua picha ya kumbukumbu kupitia libeneke la Bukobawadau
 Njia panda kuelekea Rubya nyakalembe.

Wilaya ya Muleba imetawaliwa na vilima, mabonde na tambarale (plateaus). Wilaya ipo kati ya mwinuko wa mita 1,150 na 1,667 kutoka usawa wa bahari na sehemu ya juu kabisa ni Karambi. Mto Ngono unakatisha wilaya kuanzia Kusini kuelekea Kaskazini ambapo unaungana na Mto Kagera unaomwaga maji yake katika Ziwa Victoria.
Wilaya imegawanyika katika kanda kuu nne za kilimo ambazo ni: Ukanda wa mwambao wa Ziwa na Visiwa katika Ziwa Victoria, Ukanda wa juu, Ukanda wa chini Kusini na Ukanda wa Burigi. Ukanda wa mwambao wa Ziwa na ukanda wa juu unapata kipindi kirefu cha unyevunyevu (miezi 8 – 9) wakati ukanda wa chini na wa Burigi unapata kipindi cha unyevunyevu cha miezi 3 – 4 tu kwa mwaka.
Mvua zinanyesha zaidi upande wa Kaskazini – Mashariki yaani milimita 1800 wakati Kusini – Magharibi ni pakame. Kwa kufuata viwango vya miinuko na mvua, Wilaya inakuwa na kanda za kilimo tofauti zenye mazao mbali mbali yanayopandwa katika misimu tofauti.
Hali ya rutuba ya udongo si ya kuridhisha hasa kutokana na mvua nyingi zinazosababisha kuondolewa kwa virutubisho udongoni. Hata hivyo maeneo ya mabonde ya upande wa Kusini – Magharibi na miinuko tambarale (plateaus) yana rutuba ya kutosha wakati maeneo ya mwambao wa ziwa hayana rutuba.

Njia panda kuingia mji Mkuu wa Muleba.
Pitapita za hapa na pale mida ya jioni Mjini Muleba kwa Mama Tibaijuka.
 Stend kuu ya mabasi Mjini Muleba
Kijana Nuru Mungi na mwenzake Lameck kama walivyo kutwa na camera yetu.
Mkazi wa 'AKASHOZI BUGANGUZI' akielekea mtoni kwa ajili ya kuteka maji. #Team kikwetu kwetu.
 Hali ya migomba kijijini Buganguzi
Kijijini Buganguzi 'akona'
 Muonekano  wa Kanisa la Kikatoliki  Buganguzi
 Mbatama Shule ya Msingi iliyopo kijiji cha Bushemba kata Buganguzi
Chimbuko la familia ya  Rwabizi kijijini Buganguzi
 Kijijini Buganguzi Mikungu ya ndizi ikiwa imekusanywa tayali kusafirishwa kwenda sehemu mbalimbali kwa ajili ya kupata soko.
 Maeneo ya Kasanova  kwa Tibaigana wadau wakipata moja moto moja baridi
 Kwa Tibaigana Buganguzi
Barabara ya Tan road kutoka kamachumu kuingia Buganguzi.
Eneo la gulio lililopo Katare Buganguzi Center
Ofisi ya kata Buganguzi

Mdau msomaji jiunge nasi kupitia facebook page kwa habari za papo hapo kwa ku like ukurasa wetu kwa link hii ;https://www.facebook.com/pages/Bukobawadaublogspotcom/210334185651627

Next Post Previous Post
Bukobawadau