Bukobawadau

(OKUZILIMA) NI DESTURI KWA WAHAYA

 Okuzilima ni kitendo kilichohusisha sherehe ya kijamii, ambacho familia ya wazazi wa bibi harusi ilikusanya kwa njia ya michango (okutweza) na kupeleka mali (kuzilima), hasa mikungu ya ndizi (ebitoke) na vibuyu vya pombe (amalwa), kwa familia ambako binti yao ameolewa (chini ya mwavuli wa kumzawadia binti yao). Ni wazi kwamba mila hii  ilikuza na kuimarisha mahusiano mema na maelewano ya upendo baina ya familia mbili zilizooleana.
Aidha, mila hii pia ilisaidia kujenga mshikamano katika jamii pana ya  kijiji au ukoo, kwani watu wote walialikwa na kupata fursa ya kushiriki mchakato wa sherehe kwa michango yao ya hali na mali. Kuchangia huko ndiko okutwela, wakati kuchangisha au kuhamasisha michango ni  okutweza. 
 Kwa mfano watu waliweza kuchangia mikungu ya ndizi(ebitoke n’enkundi) ili kukidhi mahitaji ya zawadi, na chakula na pombe kwa ajili ya washiriki. ‘Siku ya Siku’, watu wengine, hasa vijana, walialikwa na kushirikishwa katika misafara ya kubeba zawadi husika. Misafara hiyo ilipambwa na kukolezwa kwa  shamrashamra ya sherehe za ngoma na nyimbo (ebizina). Siku hizi, fedha zinatumika zaidi katika kufanikisha mchakato wa mila hii.
Next Post Previous Post
Bukobawadau