Bukobawadau

HALMASHAURI MKOA KAGERA ZAAGIZWA KUTOTOA TENDA KWA WAKANDARASI WASIO NA SIFA

Serikali mkoani Kagera imeziagiza halmashauri zote za mkoa huo kuzingatia sifa za wakandarasi wanao omba tenda za kujenga barabara  nakuwataka wakurugenzi wa halmashauri kutowakabidhi tenda za kazi  wakandarasi wasio na sifa wanao jenga barabara chini ya kiwango na kusababisha adha kubwa kwa watumiaji wa barabara hizo.
Akizungumza katika kikao cha bodi ya barabara kilichofanyika mjini Bukoba mbunge wa Bukoba vijijini Jonson Rweikiza amesema hakuna haja ya kuwakabidhi wakandarasi wasio na sifa katika kujenga barabara na nakuwataka wakurugenzi wa halmashauri kuzingatia vigezo na sifa za wakandarasi hao wakati wa kugawa zabuni ili kupunguza adha zinazo zijitokeza mara kwa mara na kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa madaraja ambayo yamekuwa yakitole ahadi za muda mrefu bila kukamilika. 
 
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Kagera Johni Mongera amesema atafuaatilia kimalifu suala la ujenzi wa miradi mbalimbali inayoibuliwa katika mkoa huo zikiwemo barabara na akaongeza kuwa halshauri sasa zinatakiwa kushirikina na wakala wa babara nchini Tanrods na kuhakikisha barabara zinajengwa kwakiwango kinachotakiwa ilikupunguza kero na changamoto zinazo wakabili watumiaji wa barabara. 
 
Hali hii imejitokeza kutokana na kuwepo kwa barabara nyingi na madaraja yaliyojengwa chini ya kiwango likiwemo daraja la mtoto kanoni ambalolinadaiwa limejengwa chini ya kiwango.
Next Post Previous Post
Bukobawadau