Bukobawadau

MANENO YA KAFULILA KUFUATIA HOTUBA YA RAIS KIKWETE KWA WAZEE WA DAR DEC 22,2014

From David Kafulila, Mb
1. Hoja kwamba pesa zilitolewa kwa uamuzi wa hukumu ya sept 5.2013 sio sahih ikwa sababu hukumu ilisema ALL AFFAIRS OF IPTL SHOULD BE HANDED TO PAP. Haikusema kama escrow monies ni party of affairs of IPTL kwasababu zilikuwa kwenye mgororo. hoja ya kusema hukumu ilisema ilikuja baada ya kikao cha Oct8.2013 kunduchi beach hotel ambacho kiliongeza maneno kwenye hukumu kwa kusema ALL AFFAIRS OF IPTL INCLUDING RECEIBLES FROM ESCROW AC SHOULD BE HANDED TO PAP. Huko ni kupotosha hukumu kwani hela za escrow zilikuwa na mgogoro kati ya Tanesco na IPTL na PAP kununua IPTL haimanishi mgogoro kati ya IPTL na Tanesco umekwisha bali PAP ingechukua nafasi ya IPTL kwenye mgogoro wa pesa za escrow. hili Rais kapotoshwa.
2. Kusema Muhongo atamtoa baada ya uchunguzi wake ikulu kukamilika ni mbinu ya kumlinda kwani mbona mawaziri wanne waliohusika ktk oparesheni tokomeza ripoti ya bunge ilitosha rais kutengua uteuzi wao na kisha rais akaunda tume ya rais uchunguzi. kwann kwa Muhongo inakuwa kinyume chake?
3. Bunge liliazimia mamlaka ya uteuzi ichukue hatua dhidi ya Maswi. Rais anasema suala la Maswi ameliacha kwa mamlaka ya nidhamu ambayo ni Katibu Mkuu Kiongozi, Hapa Rais amekwepa Jukumu lake kwani yy ndio anateua na kufukuza Makatibu wakuu. pia suala hili sio jipya kwa Katibu Mkuu Kiongozi ingetosha awe amekwisha kuchukua hatua za kinidhamu siku nyingi kama TRA walivofanya kwa wahusika tawi la Ilala.
4. Hoja kwamba kutaifisha mitambo ya IPTL kutakimbiza wawekezaji ina mapungufu kwasababu kwa mujibu wa ripoti ya CAG, PAP alifanya utapeli wa kughushi katika umiliki wa IPTL hivyo sio mwekezaji mwadilifu hivyo kutaifisha haiwezi kutisha wawekezaji. pia ifahamike kwamba wawekezaji wengi wanatoka Ulaya na Amerika na nchi hizo ndio zimezuia misaada kutaka serikali itekeleze mazimio ya Bunge na mazimio ya Bunge ni pamoja na kutaifisha mitambo hiyo. sasa inawezekanaje nchi hizo zinazotaka serikali itekeleze mazimio kwamba ndio zikimbie kuwekeza kwa sisi kutekeleza mazimio husika? hapa ni namna ya kulinda matapeli wanaokuja kwa jina la wawekezaji
5.Hoja kwamba mikataba ikiwa wazi itakimbiza wawekezaji ina mapungufu kwasababu tatu;
a. Nchi nyingi sasa duniani mikataba ipo wazi na mfano rahisi ni Ghana na bado wawekezaji hawajakimbikia kwasababu hiyo. Ndio utekelezaji halisi wa itifaki ya OPEN GOVERNANCE ambayo Tanzania tulisaini
b. Kipengele cha Usiri(Confidentiality clause) kwa mikataba yote kinasema mkataba utakuwa siri isipokuwa kwa pande za mkataba(parties of contract) na kwa mahitaji ya dola( statutory purpose). sasa statutory purpose maana yake ni mahitaji ya Serikali, Bunge na Mahakama. sasa tatizo la sasa ni pale serikali inapokataa kutoa mikataba kwa bunge kwa hoja ya kipenge cha usiri(confidentiality clause) wakati kipengele hicho kinaruhusu Bunge kuwa na mamlaka ya kuona mikataba kama part of state organ
c. Pia wawekezaji hawa wanaposaini mikataba hapa wanakwenda kutafuta mitaji kwenye masoko ya mitaji kwao(stock markets). Kule kwenye masoko ya mitaji wanaweka wanalazimika kuweka mikataba hiyo wazi na wanaweka. hivyo kwa dunia ya leo ni aibu kuendelea kufanya mikataba kuwa siri.
6. Hoja ya kodi. TRA walidai kodi kwa barua kwenda BOT. na Werema ndio aliandika barua kukataa kodi. Kwakuwa CAG alikiri ktk ripoti kuwa kodi ilipaswa kulipwa kiasi cha 23bn mana yake alosema kodi isilipwe anapaswa kuchukuliwa hatua za kutaka kusababisha hasara hiyo. ikumbukwe Basil Mramba yupo mahakamani mpaka sasa kwa kesi ya kusababisha hasara ya 11bb. inawezekanaje hawa waishie kujiuzulu?
7. Mwisho kauli ya Mhe Rais kuwa fedha zile ni za IPTL kwasababu tu ziliwekwa kwenye escrow na Tanesco badala ya kulipwa moja kwa moja kwa IPTL kutokana na mgogoro sio sahh kwasababu pesa ya mgogoro kati ya Tanesco na IPTL haiwezi kuwa ya IPTL mpaka mgogoro umalizike na mwenyewe amekiri kuwa mpaka pesa hizo zinatolewa mgogoro ulikuwa haujamalizika. ni kwa mantiki hiyo pesa hiyo haikuwa sahh kuita ya IPTL. pia hapa niongeze kwamba Mgogoro wa IPTL kutoza zaidi Tanesco capacity charge unamanisha ni dhuluma ya IPTL tangu mwanzo wa utekelezaji wa mkataba mwaka 2002 na sio 2006 kama Mhe Rais alivosema. Hii ni kwasababu mgogoro wa IPTL ku overcharge Tanesco kwenye capacity charge msingi wake ni udanganyifu wa IPTL ktk mtaji na hivyo hesabu yake inapaswa kuzingatia tangu mwanzo wa utekelezaji wa mkataba mwaka 2002 na sio 2006 escrow ilipofunguliwa. Hii inakaziwa na Uamuzi wa mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi wa migogoro ya kibiashara ( International Centre For Setllement Of Investment Disputes-ISCID) wa Feb12. 2014.
David Kafulila(MB)
Next Post Previous Post
Bukobawadau