Bukobawadau

TIMU YA SIMBA SC YAPATA PIGO,WANACHAMA WAKE 7 WAFA AJALINI

 Wanachama Saba (7) wa klabu ya Simba ya Dar es salaam kutoka tawi la Mpira na Maendeleo (maarufu kama Simba UKAWA) ambalo limewahi kutangazwa kufutwa wamefariki dunia katika ajali ya basi mkoani Morogoro.
Wanachama hao wakiwa katika basi lao walikuwa wakielekea Shinyanga kwa ajili ya kuipa nguvu Simba ambayo inatarajiwa kushuka katika dimba la CCM Kambarage kuikabili Kagera Sugar katika mchezo wa ligi Kuu Tanzania Bara kesho..
Vifo hivyo vimefikia 7 baada ya watano kufa palepale na wengine wawili waliokuwa majeruhi kufariki katika hospitali ya mkoa wa Mororgoro.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP Leonard Paul amethibitisha habari hizi na kusema kuwa majeruhi wamebaki 13 na kufanya vifo kufikia saba hadi majira ya saa 2 usiku wa April 03.
Next Post Previous Post
Bukobawadau